Tuesday, May 31, 2005

JIFUNZE KUBLOG MTANDAONI

KWA YOTE HAYO BONYEZA hapa

Kusoma nje ya Nchi sio lazima usafiri nje ya nchi yako!

HAYA jamani kwa wale waliokariri kusoma nje ya nchi mpaka upande usafiri kwa kupanda ndege na kwenda marekani au Uingereza hapana.

Unasoma nje ya nchi wakati uko ndani ya nchi, na unapata Digree kwa muda wa miezi michache kama alivyonena kaka yangu hapa Bw. R.s Miruko.
kama unabisha bonyeza hapa.

Saturday, May 28, 2005

WANAWAKE BWANA...........! YAANI AKULETEA VIRUSI NA UNAVIPOKEA KWA MIKONO MIWILI

KAMA mkeo au mpenzi wako anatoka nje ya ndoa na unajua kabisa yaani una uhakika utafanya nini?

Jibu la swali hili kwa wanaume wengi litakuwa ni lenye kuashiria maumivu kwa upande wa pili.

kwa vipi sasa?

jibu linaweza kuwa nitamwacha hapahapo au nitamwua ama tutakufa wote mimi na yeye, hayo yanweza kuwa majibu toka kwa mwanaume ambaye amefahamu hilo.ni amjibu ambayo ni ya kishujaa eh!

iwapo mwanamke angeulizwa swali hili unadhani angelijibu vipi?

bila shaka angelijibuhivi; 'nitaondoka au nitamkomesha huyo hawara yake ama shauri yake mwenyewe mimi si nitaendelea na maisha yangu' haya ni majibu muafa ya kinyonge eh!

kwa kawaida wanaume hawako tayari kusamehe kosa la kutoka nje linapofanywa na wake au wapenzi wao, ni wachache sana wanaoweza kusamehe.

sisemi kwamba hakuna wanawake ambao nao huchukulia kutoka nje kwa waume zao kama jambo lisilo sameheka, kiwango cha wanawake hao ni kidogo sana ikilinganishwa na kile cha wanaume ambao hawako tayari kusamehe uzinzi wa wake zao ama wapenzi wao.

wanaume saba kati ya kila kumi hutoka nje, tafiti zinaonyesha kuwa wanawake karibu watano katika kila kumi wanajua kuwa wanaume wao htoka nje lakini huwa hawana la kufanya, wameamua basi!

alkini wanawake wanane katika kila kumi wanajua kwamba waume zao wanatoka nje na wanachukua hatua za kupambana na hali hiyo wakiwa ndani ya ndoa zao, wakati ni mwanamke mmoja katika kila wanawake kumi ndiye huondoka kwenye ndoa ya aina hiyo. hii siyo taarifa nzuri kwa akina mama.

KUKUBALI kuishi kwenye ndoa ambapo una uhakika kabisa kwamba mwenzako anakwenda nje kutafuta kifo huku akikufuja kwa njia moja ama nyingine ni kujishusha sana, kuna wale wanaosema shauri lake kwa sababu wameshakubali kwamba wao ni watumwa wa hao wanaume bila kufikiria.

hivyo wana haki ya kupangiwa nao hata siku ya kifo, hapa wanawake na wasichana ni lazima tuwe macho na tuamke sasa tukiendelea kuishi maisha ya namna hii matokeo yake tutakuwa tunasubiria kuletewa virusi vya UKIMWI na tunavipokea kwa mikono miwili na badae tunakufa kwa ugonjwa wa Ukimwi kwa madai kuwa Mungu katutenganisha.

Wednesday, May 25, 2005

Wachungaji hawa walichunga sana Kondoo wa Bwana.!

Eee baba Mungu wabariki hawa Nguchiro wafanikiwe kwenda kwenye adhabu yako ya milee wakiwa kama kuni katikakatika ya mafiga ili waungue vyema kutokana na kuudanganya uma kuwa wao ni wachungaji wa kondoo, AMEN.

Tuesday, May 24, 2005

TLP! Ni kaaazi kwelikweli.............!!!!!!!

HAKI ya Mungu yaani Chama cha Tanzania LabourTLP kina mbwembwe kweli kweli! Zile za CCM ni cha mtoto wanawake sasa sawa na wanaume yaani wee acha tu.

ni kwamba hivi karibuni chama hicho kimemsimamisha mgombea mwenza wa urais mwanamke ambaye atakuwa akigombea nafasi hiyo na Mwenyekiti wa chama hicho Bw. Augustino Lyatonga Mrema mwezi oktioba mwaka huu.

basi bwana wamemsimamisha mwanake awe mgombea mwenza wa nafasi hiyo kwa madai ya usawa unazingatiwa katika chama hicho ambacho hivi karibuni tuu kimepata ruzuku baada ya msajili wa vyama vya siasa nchini Bw. Tendwa kutangaza kuwa anakitambua chama hicho.

lakini sasa huyo mgombea mwenza anavigezo vya kuwania nafasi hiyo?

kwa kuzingatia yafuatayo wenyewe mtasema kama vigezo anavyo ama laa!

* Je Ikulu ni Maabara ya kufanyia majaribio ya uongozi?
* Ikulu ni mahali patakatifu amejitakasa?
*kazi ya urais si ya kubeba zege Bongo yake inachemka?
*utamu wa komamamnga ni komamamnga lililokomaa, amekomaa?

Angalizo: USHUZI HAUZIMI MOTO! Mnakaribishwa kuchangia maoni yenu bila woga wala Jabza na kutopendelea kwa aina yoyote, karibuni sana.

Friday, May 20, 2005

Takrima ni tatizo la Kimaumbile

Najua kila mtu ana hamu ya kulifahamu hili kwa undani kwa nini takrima iwe tatizo la kimaumbile ni maelezo machache tu hapa mda mchahe utakuwa umeelewa.

ni hivi ; kwa mujibu wa mila na desturi za kitanzania ni kwamba mtu anajikuta mwili unamuwasha kila anapokuwa anasalimiana na wenzake hapa naamanisha viongozi mbalimbali hapa kwetu tanzania.

hii inawatokea mara nyingi katika nyakati mbalimbali na hasa katika nyakati hizi ngumu za uchaguzi pale wanapojiandaa kutafuta kura katika kampeni zao.

anajikuta mwioli unamuwasha, anajikuna kwa staili ya kuingiza mkono mfukoni akitoa anatoa burungutu la pesa, anawagawiwia wapambe na wapiga kura akiwa hajitambui kabisa kuwa anawashwa anajikuna kwa staili ya aina gani.

akimaliza kujikuna anarudiwa na fahamu na kukumbuka kuwa alitoa burungutu la pesa na kuwagawia watu mbalimbali na kugunduia kuwa ametoa takrima, basi tena ndo matatizo ya kimaumbile na staili za kujikuna pale unapojisikia uanawashwa.

TAKRIMA NI TATIZO KUBWA SANA LA KIMAUMBILE SASA ANATAFUTWA DAKTARI BINGWA WA MAGONJWA YA NGOZI ASAIDIE KUTATUA TATIZO HILI KWA WATANZANIA KWA KUSHIRIKIANA NA TAKURU.

Tuesday, May 17, 2005

Itafika wakati hata Jogoo watawika Kwa Lugha ya Kiingereza!

Tangu enzi za mababu zetu watanzania tumekuwa tukijitahidi kuenzi utamaduni wetu na hasa baada ya kupata uhuru wetu mwaka 1961 chini ya Mwl J. K. Nyerere wee acha tu.

licha kuwepo kwa juhudi za kuuenzi utamaduni wetu wa kitanzania pia kupitia lugha yetu ya taifa ya kiswahili tumekuwa tukiitumia sana katika kuuenzi utamaduni huu kuanzia katika shule za awali hadi vyuo vikuu.

kutokana na watanzania wengi kujitahidi kuendeleza zoiezi zima la kuuenzi utamaduni wao kumekuwapo na vikwazo kibao ambavyo vimekuwa vikiwafanya watanzania hawa kushindwa kuendelea katika suala la kuuenzi utamaduni kutokana na baadhi ya viongozi wao kukazia kutumika kwa lugha ya kiingereza.

kutokana na watanzania kukaririshwa kuwa kiingereza ni lugha ya kimataifa na kutokana na tanzania kufikiria tena kuingia katika shrikisho la jumuiya ya nchi za afrika mashariki hapa watanzania wamekuwa wakichanganyikiwa sana.

kinachowachanganya ni kuhusiana na hiyo lugha wanayoambiwa kuwa ni ya kiamtaifa kama huijui huwezi hata kufanya biashara ya kuku nje ya nchi, kikubwa zaidi kinachowachanganya watanzania wanaoishi kule mvumi kuhusiana na wao kufanya biashara nje ya nchi wakati hata 'kiswakigo' (kiswahili Kigogo) chenyewe kimepita kushoto.

lakini kinachowachanganya zaidi ni suala la kuwafundisha mbuzi wao wanaotegemea kwenda kuwauza nje ya tanzania jinsi ya kulia kiingereza au jinsi ya kuwafunda kuku wao jinsi ya kuwika kiingereza wanapokuwa katika masoko nje ya Tanzania.
Itakuwa ngumu sana kufamnikiwa katika suala la kuuenzi utamaduni wa mtanzania kupitia katika lugha ya taifa ya kiswahili huku viongozi wakisisitiza kuwa kiingereza ni lugha ya kiamataifa, umefika wakati ambapo mataifa mengine waambiwe kuwa kiswahili ni lugha ya kiamataifa.

ili nao waanze kuwafundisha kuku wao kuwika kokoriiiko yaani kwa kuwika katika lugha ya kiswahili au waanze kuwafundisha mbuzi wao kulia kwa lugha ya kiswahili Meeemeeeee! ili tufikikie malrngo ya kuuenzi utamaduni kama wao walifanikiwa.

Monday, May 16, 2005

Ukitaka kwenda mbinguni lazima upitie nji hii hapa

Ni kuzuri sana, lazima upapitie hapa kabisa usipopitia hapa ujue unakwenda kwingine. Kong'oli hapa!

Ndoa ni kazi Ngumu lakini ni Muhimu, kwa nini wengine hawaowi au kuolewa?

Ndoa ni agano linalowekwa kati ya mwanaume na mwanamke wabatizwa mbele ya Mungu ili wawe mke na mume.

Kwa mujibu wa Maandiko Matakatifu, agano hili linawafanya wabatizwe wawe mwili mmoja wakishiriki haki zote za ki-ndoa pamoja na mafao ya kijamii yatokanayo na hali ya ndoa.

sasa ni kwa nini wengin hawaowi wala kuolewa, Bofya hapa!

He! Kumbe kuna watu wanakunywa pombe kila siku lakini hawafahamu bei yake........

Ni ngumu kuaminishwa lakini utakaposhuhudia ni lazima ukubali kuwa ni kweli yanatokea.

hii kwa wale wahudumu wa sehemu zinazouzwa Pombe yaani 'Bar wanalitambua sana hili na wala sio geni kwao kutokana na uzoefu wa kazi yao ya kuuza bia kwa watu mbalimbali.

wahudumu wao ambacho hujali ni kulipwa pesa zao haijalishi pesa hiyo ni ya wizi au ya kuhongwa kitu ambacho kimekuwa kikiwagharimu wanunuaji au walipaji wa vunywaji husika.

hapa kubwa ninalolizungumzia ni kuhusiana na tabia ya baadhi ya watua mabo kila mda ukikutana naye kila muda yeye amelewa tu halafu kabla ujamuuliza utasikia anakwambia niko pombe anadhani ni sifa kubwa mbele ya watu anaowambia.

lakini cha kushangaza ni kwamba mtu huyohuyo ukimuuliza umekunywa ngapi kwa sauti kubwa atakujibu harakaharaka nimekunywa kumi, na ukimuuliza ni sawa na kiasi gani cha pesa alichotumia utamuona anainama chini kana kwamba anafikiria kitu cha maana badala yake anakujibu SIJUI.

NI hatari sana kwa wale wenye tabia hii hususani ni akinaada ambao kutwa yuko pombe ukimuuliza bei ya bia moja hajui ni kiasi gani akian kaka nao tabia hii ni hatari sana zaidi kuliko kwa akina dada, lakini haya si mawazo yango hata R.S analitambua hilo.

Hebu tuweni na ustaarabu jamani hata kama unapewa ofa kila siku basi siku moja pita mwenyewe bar ujaribu kuulizia bei tu ya bia kama unavyofanya kwenda dukani kuulizia bei ya kiatu au nguo ili uwe na uhakika wa ofa unazopewa mtaani.

Monday, May 09, 2005

Ni kweli kuwa CCM ya Mkapa ni tofauti ile ya Nyerere?


haki yangu Mungu siasa ni mchezo mtamu sana, lakini mambo yanapokugekia utatamani ardhi ipasuke uingie ndani ili watu wengine wasikuone, wapinzani nao wana mambo Soma hapa

Wengine walishehekea hivi Siku ya mama!

Tarehe 8 May kila mwaka duniani kote husherehekea siku ya mama Yaani Mothers Day!

hapa kwetu Tanzania watanzania nao pia walisherehekea siku hii kwa furaha kubwa ikizingatiwa siku hii iliangukia katika siku ya Jumapili ambayo ni siku ya mapumziko ya mwisho wa wiki.

wengine walisherehekea siku hii kwa kuwashukuru mama zao kuwaweka hapa duniani kwa kuwazaa, kuwalea na kuwapatia kila kilicho mahitaji yao na kuwafikisha hapo walipo sasa.

wengine waliwapatia mama zao zawadi mbalimbali ikiwemo kadi, maua na zawadi nyinginezo nyingi kwa ajili ya kuonyesha upendo wao halisi kwa mama.

lakini kwa upande wa wa wafanyabiashara hali kwao ilikuwa tofauti na wengine kwa kuwa wafanyabaishara wao walikuwa wakifanya biashara kwa kuuza kadi za siku ya mama na maua kwa ajili ya siku hiyo.

mwanzilishi wa siku hiyo Bibi. Anne amekilaani kitendo hicho cha kufanya biashara kwa kusema kuwa kuwa lengo la siku hiyo halikuwa kufanya baishara kama wanavyofanya sasa watu wengi hapa duniani.

anasema kuwa lengo la kauzishwa kwa siku hiyo ni kuwapongeza akina mama ambo walikuwa wakiwapokea waume zao ambao walikuwa wakirejea kutoka vitani ambao kabla ya kuondoka waliawaacha akina mama hao wengine ama wakiwa na watoto wadogo ama mimba ambazo akina mama hao pamoja na kupata shida zote za upweke waliweza kuwalea watoto wao na kaundaa mapokezi kwa ajili ya kuwapokea waume zao ambao walikuwa wakitoka vitani.

upendo huu waliouonyesha akina mama hawa ulisababisha kuanzishwa kwa siku hii muhimu sana na siyo kwa ajili ya kufanya baishara kama ilivyo sasa. HONGERENI AKINA MAMA!

'FIRST LADY' Huyu hakupata kitchen Party kabla ya Kuingia Ikulu?



KILA mtu anaamini kuwa Ikulu ni mahali patakatifu na kila anayeingia Mahali hapo alzima awe ametakaswa kabla hajaingia, licha ya kuwa ni ngumu mtu kutakaswa kabla hajafa.

suala la kujitakasa pia ni zuri na hasa kwa akina mama ambao wana madaraka makubwa ya kuwaongoza wenzao au akina mama ambao waume zao wana madaraka makubwa hii ikiwa ni pamoja na kuwa mke wa rais.

nawapa pole sana wenzangu wakenya, hapa naamanisha watu wote wanaoishi kenya Afrika mashariki hii ambayo tunategemea kuwa na Jumuiya ya afrika mashariki kwa kuchangia kila kitu hususan katika masuala ya biashara.

pole hii hasa ni kwa akina mama wa kikenya, nawapa pole sana hawa kwa kuwa mke wa rais waoamekuwa akifanya mambo ya ajabu ikiwa ni pamoja na kushinikiza mumewe kufanya mambo ya ajabu ajabu kutokana na mumewe kuwa na cheo cha juu cha utumishi kuliko vyeo vingine hapa afrika.

mama huyu licha ya kufanya mambo ya ajabu hivi akribuni alitoa kali baada ya kuvamia chumba cha habari cha gazeti moja la nchini kenya akitaka kuombwa radhi kutokana na gazeti hilo kumuandika.

licha ya kuvamia chumba hicho cha habari pia mama huyo alimpiga vibao mpiaga picha wa gazeti hilo kwa madai kuwa alimpiga picha!

sasa mablogist wanawake wenzangu kwewli hii ni haki? mwanamke mzima mwenye akili timamu na mumeo ni mtu mwenye madaraka ya juu unafanya mambo kama mtoto mdogo anayesoma vidudu?

poleni sana akina mama wa kenya huyu mwanamama amewadhalilisha sana akinamama wa kenya kwa tabia yake hiyo ya ajabu kwa kufanya hivyo watu wa mataifa mbalimbali wamefikiria kuwa wanawake wa kabila lake wote wako kama mama huyo alivyo. pole sana First Lady! milango iko wazi kwa ajili ya kuchangia maoni yenu kuhusiana na tabia ya mama huyu wa ajabu karibuni wanablog.

Saturday, May 07, 2005

Kaguo alamba Ugombea wenza 2

kutokana na sababu za kiufundi habari hii haikuweza kusoma vilivyo lakini sasa mambo yanaenda kama yalivyopangwa.Kong'oli hapa

Thursday, May 05, 2005

MAPAPARAZI wapewa vitambulisho vya Wahudumu!

Waandishi wa habari ni watu muhimu sana hapa nchini na duniani kote kwa ujumla na wengi wamekuwa wakiita fani ya uandishi wa habari kuwa mhimili wa nne!

lakini watu hawa wamekuwa wakionekana kuwa hawana maana sana na hasa pale wanapoalikwa katika shughuli mbalimbali za kitaifa.

Ni hivi karibuni mjini Dodoma kulimalizika tukio kubwa ambalo lilikuwa linakamilisha neno kutimia ambapo wana CCM walikuwa wakiteua mgombea urais ambaye wengi wanaamini huyo ndiye rais wa awamu ya nne.

katika mkutano mkuu huo maalum wa CCM wageni wengi toka ndani na nje ya nchi walialikwa kwa ajili ya kuhudhuria mkutano huo wakiwemo waandishi wa habari toka vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini.

licha ya kualikwa kwa wageni wengi na waandishi pia, wageni hao walitafutiwa mahali pazuri pa kulala na kupewa kadi maalum za kuingilia katika ukumbi wa mikutano wa CHIMWAGA.

kinyume na wageni wengine waandishi wa habari hawakupewa uzito kama ilivyokuwa kwa wageni wengine ambao walialikwa kuhudhuria Mkutano huo na badala yake walionekana kama wafanyabiashara wa nguo toka mikoani.

siku ya mkutano baadhi ya waandishi wa habari walionekana kukosa kabisa kadi hizo maalum ambazo walitakiwa kuwa nazo na kuwaruhusu kuingia katika mkutano huo maaluma ambao ulikuwa na ulinzi kupita kiasi.

baadhi ya waandishi wa habari na wapiga picha ambao walibahatika kunusa milango ya ukumbi huo walipata kadi za uhudumu wa Vinywaji na vyakula ambazo zilkuwa zinatumiwa na wauzaji wa vyakula na vinywaji nje ya ukumbi huo.

hii iliniuma sana, mbaya zaidi ni pale matukio muhimu yaliyokuwa yakitokea ndani ya ukumbi huo yalikopokuwa yanafanyika wapiga picha na waandishi wa habari walitakiwa kushuhudia ili kuwapa taarifa wananchi ambo wako tandahimba.

ilikuwa ngumu kwao kuingia kutokana na vitambulisho vyao kuwaruhusu waandishi na wapiga picha kuishia nje ya milango ya ukumbi huo.

kilichokuwa kinagomba hapa ni kwamba baadhi ya maafisa wa usalama walikuwa wakiwaambia waandishi hawa kuwa "nendeni mkawahudumie huko nje huku ndani tuko kamili"

licha ya kunyimwa vitambulisho pia walifukuzwa katika nyumba za kulala wageni amabzo walikuwa wamefikia kwa madai kuwa CCM ilikuwa imezikodi nyumba zote kwa ajili ya kufikia wajumbe wa Cma hicho.

hii inaonyesha ni jinsi gani waandishi wa habari wasivyothaminiwa katika jamii hususan na baadhi ya viongozi wa Chama cha mapinduzi katika idara ya habari.

CCM kama hamuyawezi waachieni Idara ya habari maelezo watayamaliza wao bila kufanya hiyana kama mliyofanya katika mkutano wenu mlitukwaza sana.

Tumewasamehe na tumemkemea Pepo mchafu aliyemo nsdani ya chama chenu katika jina la Yesu ashindwe na asiendelee kuwepo! AMINA.

Ni moshi wa kijani lakini sio wa Mjomba.............!

HAYAWIHAYAWI sasa yamekuwa, jana mosho wa kijani ulifoka katika ukumbi wa Chimwaga na kuwamwaga wale 2 ambao walitakiwa kumwagwa haraka sana kabla Jogoo halijawika.

hatimaye jana neno likatimia! shangwe na vilelegele vifijo na Nderemo nguo za kijani, moshi wa kijani hii ilikuwa ikimaanisha sasa Imekwisha.

kilichonitia wasiwasi ni pale Moshi ule wa kinai uliotoka na kuonnyesha aliyekuwa amechaguliwa ni mwingine siyo mjomba wangu! hapa ilikuwa ni ngumu kuamini lakini baadaye fahamu ziliponirudia nikaamini kuwa ni kweli hakuwa Mjomba.

lakini kwani huyo na mjomba wana togfauti gani hapa nilijiuliza na kukosa jibu kabisa lakini nilipomuuliza Binamu akaniambia kuwa eti mjomba alikuwa Mzee sana kuliko huyo mteule.

nikamuuliza Binamu kwani Ikulu kuna kazi za kubeba Zege? akanijibu kuwa hata kama kazi si za kubeba zege lakini huu ni muda wa vijana kuonyesha ujana wao katikia wakati wao wa ujana hususan ni kipindi hiki.

sikuishia hapo nikamuuliza tena; kwani ukienda katika kijiji ambacho umgeni sana utatafuta kijana maarufu au Mrembo maarufu na kuuliza shida yako?

akajibu hapa, nikamuuliza tena utumtafuta nani na kumuuliza? akijibu; nitamtafuta Mzee maarufu na kumuuliza.

hapo nikaridhika kumoyo! nataka kukwambia Binamu kuwa sasa kwa taarifa yako Mjomba amekata rufaa! na Ikulu hakuna kazi ya kubeba Zege na utamu wa embe ni lile ambalo limeivia juu ya mti siyo la kuvundika.

Kaguo alamba ugombea Mwenza

Waandishi wa habari nao hawako nyuma kwa Vituko na hiki ni kimojawapo kati ya vituko hivi! Soma hapa

"Hata nisipochaguliwa nitarudi kuwashukuru"

Hapa namnukuu aliyekuwa mmoja kati ya wale wanaiomba CCM kumteua kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho alipokuwa akirudisha fomu ya kuomba baraka hizo

Mgombea huyu alisema kuwa iwapo hatobahatika kupata nafasi hiyo ya kuteuliwa na kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho basi angerudi katika mikoa yote 26 aliyozunguka wakati akiomba wasdhamini kwa ajikli ya kumdhamini katika suala zima la kupata baraka za kuteuliwa kuwa mgombea urais.

alisema kuwa angerudi na kuwashukuru wale wote waliomdhamini na kuwataarifu matokeo juu ya kile kilichotokea katika uteuzi huo.

swali? je ni kweli atafanya hivyo!

nafikiri itakuwa ngumu sana kwanza bado anazo nguvu za kwenda huko kuzunguka na kuwatafuta tena wadhamni wake na kuwakatia takrima kama alivyofanya hapoa awali alikwenda kuwabembeleza kwa ajili ya udhamini?

nasubiri sana huu wimbo urudiwe kuimbwa na mwasiasa huyu ambaye alipokuwa akiyasema haya alionyesha ujasiri wa hali ya juu kana kwamba alikuwa an uhakika wa kuwa mteule katika nafasi ya kuwa rais mgombea.

haya tunakusubiri kwa hamu sana baba! wadhamini pia wana hamu ya kujua yaliyokusibu mpaka ukachinjwa na kutupiliwa mbali.

WELCOME BACK utupe FEEDBACK!

Monday, May 02, 2005

Kuzirai ni Muhimu lakini Kulia kwa Wabarabaig ni Mwiko

Najua huwezi kuamini lakini jinsi hali inavyooneka ndivyo itakavyokuwa, ni ngumu kuamni lakini ukweli utabaki kuwa palepale, hao 10 kati yao wengi watalia, lakini inawezekana 9 tu ndio watakaolia huyo 1 itakuwa ngumu KULIA anaweza akazirai na kupoteza fahamu lakini asidondoshe hata chozi kutokana na imani za huko kwao Mbulu.

Hayo yatakuwa ni matokeo tu na ukweli utabaki kuwa palepale!

TOP 5 wa sensitine ndogo ya Nec hawa hapa!

Haki ya Mungu yaani huwezi kuamini mambo CCM yaani chama cha mapinduzi, watu wote sasa masikio yao na akili zao zote zimeelekezwa mjini Dodoma kwa ajili ya kujua ni nani atakayepigana kiume kufa na kupona kwa ajili ya kumrithi Mkapa.

Kubwa ambalo hata wenyeji wa mkoa wa Dodoma ambao pia nao ndi wanaishi hapa mbado wana hamu ya kuwafahamu hao waliofanikiwa angalau kuonja kidogo hayo ambayo kwa pia wanahisi ni mafanikio ya kuanza safari ya kwenda Sensitine Kubwa ya Chimwaga.

akina mama nao hawako nyuma, wako msatari wa mbele kwa ajili ya kufanikisha akina baba ambao walijitokeza katika kuonja majaraibio ya kinyan'ganyiro hicho wanafanikiwa na wao kuitwa 'FIRST LADY' licha ya kuwa wao waliogopa kluchukua fomu na kuongozana na waume zao ambao hapo baada nafikiri wangeitwa 'FIRST GENTLEMAN'

mpaka sasa wachezaji 11 wako uwanjani wakiongozwa na golikipa Babu Ushindi ambaye kwa mujibu wa wataalam wa mambo ya siasa anatisha kimsingi.any way kesho utawafahamu hao TOP 5! USIKOSE!

Sunday, May 01, 2005

Wanawake wasubiri 'moshi wa kijani' Chimwaga

Licha ya ukweli kuwa hakuna hata mmoja aliyejitokeza kwa ajili ya kuwania kuteuliwa kuwa mgombea wa kiti cha urais kwa tiketi ya CCM, bado wanawake nchini Tanzania, kama walivyo Watanzania wengine watakuwa wakisubiri kwa hamu kujua kuwa baraza la mapapa wa CCM litafukiza moshi wa aina gani baada ya vikao vyao vitakavyofanyika katika siku tatu zijazo mjini hapa.

Kwamba kutatoka moshi wa aina gani, hilo sio swali ambalo mtu anaweza kulijibu kwa haraka sana hasa kwa kuzingatia kuwa karibu wagombea wote wana nafasi sawa ya kuweza kushinda licha ya tambo, mbwembwe na madoido ya hapa na pale yaliyoshuhudiwa toka kwao toka walipochukua hadi kurudisha fomu.

Je ni moshi wa kijani, wa njano, kijani na njano, moshi mwekundu kama alivyosema kakayangu Kulangwa au ni cheche kama alivyosema kaka yangu Rama? Swali hili litajibika hivi karibuni baada ya baraza la mapapa wa CCM kukutana pale 'Sestine' yao (Chimwaga). Tuombe kheri na Mungu atuongoze.