Tuesday, June 28, 2005

Monday, June 20, 2005

Mila Hii itawamaliza Wamasai 'Katatumaliza Jamani'

WAMASAI ni kabila moja kubwa sana, na ni kabila moja ambalo limekuwa likijitahidi kuenzi na kudumisgha mila na Destutri ya kabila hilo hapa nchini.

Licha ya kufanya hivyo wa mila zao wamekuwa wakidumisha kwa staili ya ajabu hebu kaa mkao wa kula ushangae ya Musa.

MILA hii katika kabila la kimasai inawalenga vijana ambao wamekwishaoa ambao rika lao linaitwa MORANI.

MILA hii iko hivi yaani MORANI wa kimasai anapojisikia kufanya Ngono anakwenda katika nyumba yoyote ambayo ni kijana mwenzee mwenye mke.

Kabla hajaingia ndani ya Nyumba hiyo anachomeka Mkuki wake mlangoni halafu akiingia ndani anamkuta mama mwenye nyumba wanaanza kufanya Mapenzi.

Kila mtu anajua kuwa umasaini hakuna mipira ya Kiume yaani (condoms) wanashughulika bila kutumia zana ya aina yoyote hapa.

wakati wakiwa ndani wanafanya mambo hayo Baba Mwenye Nyumba akija anakuta Mkuki uko nje ya Nyumba yake anachofanya ni kuondoka zake na kuwaacha Adam na Eva wanafaidi Tundi.

Unajua akitoka hapo anakwenda wapi? akitoka hapa na yeye anakwenda katika Nyumba nyingine ambayo ana uhakika akienda atafanya kile ambacho mkewe anafanyiwa anafika anachomeka Mkuki nje anaanza kuvunja amri ya sita bila zana!!!!!!!!!!1

Sasa fikiria ni wamasai wangapi wapo Jijini Dar Es Salaam wanafanya kazi ya Ulinzi na wafanya Ngono na machangudoa wa kule Kinondoni kwa pesa ambazo wanapata.

Wakirudi umasaini wanagawa Virusi bila kujua kuwa wanavimiiliki ndani ya miili yao kwa wake wa wenzao ambao nao watavipata bila kujua kwa wake wa wenzao.

Kamchezo kazuri sana lakini kamejaa rafu za ajabu, yani hakuna refa wala mshika kibendera na mbaya zaidi hakuna hata wale wahudumu toka msalaba Mwekundu (RED CROSS), yaani ukichezewa rafu hakuna cha huduma ya kwanza wala nini!

Sasa kama tukidumisha Mila zetu kwa staili hii ni nani atabakia katika Tanzania hii ambayo uchumi umekua kwa asilimia 4?

Wakati umefika sasa tubadilike kuendana na Karne ambayo sasa ni Sayansi na Teknolojia na hatuko kabisa katika Zama za Mawe za Kale ati ee.

NGO's, CBO's na Serikali hebu iangalie suala hili kwa ukaribu zaizi katatumaliza haka ka UKIMWI jamani kwa kudumisha mila kwa sataili hii.

Sina hakika kama TACAIDS wana habari hii hebu walifuatilie basi hili jamani.

TAKE CARE!

Friday, June 03, 2005

Kwa nini wasanii hawa washike mbele tu kunani? mnamfundisha Junior tabia Mbaya..

OO! mziki wa kizazi kipya unakua! unakua kwa vigezo gani? hebu anganlia mambo yanayofanywa na wasanii hao halafu uchangie unakua kwa vigezo gani na kiwango kipi!

kwa nini iwe mbele tu? na siyo Kwenye mataa ya Koo? kwa nini washike mbele tu tena kwenye nanihii na isiwe mgongoni au kuyakumbatia kabisa mabega?

kwa nini wasanii hawa hupendelea kushika sehemu za siri na kuziminya kana kwamba zimewakosea kwa kiasi kikubwa na wanatoa adhabu?

ndivyo mziki wa kizazi kipya unavyokua kwa kufanya mambo ya ajabu ajabu tena kwa kuiga toka kwa akina P. Diddy na wenzie kina Snoop DogDog.

Ina maana akina P. Diddy wakila V-nye-C na wao watakula vya kwao? hayo si ndo mambo ya kuiga? si twaigan kila kitu toka magharibi? Wao washike nasi tushike ? wao wakisema Maza faka nasi twasema baza faka!

wakitembea mataa ya koo nje nasisi tutembee mataaa ya koo wazi eti tu kwa kuwa P. Diddy kaacha yake nje? utamaduni huu umeanza lini kwetu Tanzania?

Mjinga atakwambia huu ni ushamba, kwani mkiimba huku mnapeperusha mikono kama mnataka kupaa mbinguni bila kuipeleka kusini mziki hautachezeka?

Si mshike basi hiyo maiki kwa mikono mikono miliwi? mbona kuna staili nyingi tu za kucheza vizuri bila hata ya kumsumbua huyo jamaa?

kama mmeshindwa kubuni staili nyingine ni bora tu muwe wastaarabu kama mnacheza ngona ya Mganda maana hii ndiyo asili yetu watanzania.

huu ni ushauri wa bure kwenu nyie vijana wa vizazi vipya, kama hamtaki mtajiju, na kushikashika kwenu huko WALAH! mtajikuta siyo ridhiki!

Mnadhani huyo jamaa anapenda kuchezewa ovyo? Mazingira, tamaduni na makuzi yetuhayako hivyokizazi kinateketea kimaadili huku wanajua kuwa wanayoyafanya si mema machoni pa watu.

makabila mengine wanapoona mnashika hivyo kwao tafsiri yao ni matusi makubwa ya nguoni sasa mnafikiri watakuja hata kwenye hayo matamasha yenu watukanwe?

Badilikeni basi vijana wenzangu kwa kuwa huo mziki wenu hata mimi naupenda sana lakini naogopa kutukanwa pale mnaposhika chini, acheni kumfundisha Junior Tabia mbaya.

wasanii wa kizazi kipya na kile cha zamani bila kuwasahau wasomaji wote mnakaribishwa kutoa maoni yenu bila jazba wala upendeleo wa aina yeyote karibuni sana!

Wednesday, June 01, 2005

Kutoka Ugogoni

Hii ndio asili halisi ya Jina 'MATONYA'

AGWEE! MATONYA ta uze ahano luluhaba ukuchemwa siukusaka kuza, Sunheee!
WEE MAMVUA hebu njoo sasa hivi kwa nini unaitwa hutaki kuja? fanya haraka!

Jina la matonya ni maaruu sana hapa nchini watu wengi wakitajia matonga huwa wanahamisha mawazo yao na kufikiria mkoa wa Dodoma yaani naanisha UGOGONI!

Matonya ina maana kubwa sana na hasa wale wenyeji wa mkoa wa Dodoma wanalifahamu hili kwa sana! yaani wanajua kuwa kama hakuna matonya lazima mwaka huo kutakuwa na njaa.

Matonya ni mvua nyingi za masika mabzo zinanyesha kwa fujo katika kipindi cha msimu wa mvua husunani katika mikoa ya kanda ya kati.

Ni kipindi cha masika yaani mvua zilikuwa zinanyesha kama hazina akili nzuri vile.

Na mara nyingi watu wa majina haya huwa ni wanaume ambao ni akina matonya, lakini kwa upande wa wanawake waliozaliwa katika kipindi hiki huitwa 'Mamvula' yaani mamvua.

Agwe Leche Duh! wala sijakutukana naanisha wee acha tu! watu wenye asili ya majina haya hutokwa sana na jasho katika muda wote wa maisha yao.

Hutokwa na jasho katika wakati wa baridi na hata wakati wa joto wao hutokwa na jasho, awe mwembamba au mnene yeye anatoka jasho kwenda mbele yaani kwa ufupi hutaniwa kuwa wana afya sana.

Sasa nafikiri mpaka hapa kila mtu ameshaelewa nini maana halisi ya jina hili kwa kuwa kila jina lina maana yake watu wengi wamekuwa wakiyakataa majina yao ya asili na kusahau kuwa huo ni utukufu wa kimila.

Jivunie kabila lako kqwa kudumisha mila ili upate baraka na heri nyingi duniani!