Wednesday, July 27, 2005

KHA! Akina dada Tumelaaniwa au?


NAJUA, kuwa kila mtu anayetyembelea Web Page yangu anafahamu kuwa ni nini naongelea zaidi katika kila kurasa.

Sasa hili nililokutana nalo linaniytia uchungu sana, inaniuma sana ninapoona akina dada wenzangu wanafanya mambo ya ajabu wakati wamejaaliwa kila kitu yaani wamekamilika kila Idara.

Hebu angali sasa ni nini hiki? inaiuma sana kuona akina dada hatujithamini kabisa miili yetu, eti siku wanasema wapewa bure na lazima wapewe bure wewe usijidanganye kwa hilo na ulaaniwe.

Huyu ukimuuliza ni nini anafanya hapo atakwambia yuko kazini lakini hiyo kazi yako ya kucheza shoo ukivaa vizuri mbona itanoga tuuu? kilichomsibu sasa Soma hapa chini.


Mr Nice nusura amtwange mnenguaji wake!

MWANAMUZIKI mahiri katika miongoko ya Takeu ya kizazi kipya Lukas Mpenda almaarufu Mr Nice Ijumaa iliopita alimkwida mnengaji wake aliyetambulika kwa jina la Mpasi Mussa nma almanusura angemtwanga makonde.

Tukio hilo lilitokea kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa bendi ya Msondo Ngoma Music ambayo zamani ilikuwa ikiitwa OTTU Jazz. Mr Nice alimkunja mnenguaji wake akionekana kapndwa na hasira kitendo kilichofanyika nyuma ya jukwaa la ukumbi huo uliokuwa umehudhuria na mashabiki wengi.

Mr Nice alizua tafrani hiyo kwa madai kwamba mnenguaji wake huyo alikosa nidhamu kwa kudai pesa yake kwa utaratibu aliodai haukuwa wa heshima. "Inabidi nikuonye kutokana na utovu wa nidhamu ulioufanya, nakuonya kama mdogo wangu," alisikika akifoka Mr Nice.

Hata hivyo menguaji huyo aliomba msamaha na ndipo Mr Nice alipomwachia huku akisikika akimwambia: " Mimi sipendi kufanya kazi na watu kama nyinyi, sitaki kuwa pamoja na wewe kwa sababu umenidhalilisha."

Acha kazi kwani lazima ucheze Shoo? anza hata kuuza Vitumbua au Maandazi ukiwa na Msimamo maisha yatakunyookea mwenyewe utashangaa huwezi kuamni.

Haya kila la Kheri

Monday, July 18, 2005

Wizara Nyeti ambayo Waheshimiwa Wabunge hawaifahamu!!!


WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII

WIZARA ya Maliasili na Utalii ni Wizara NYETI ambayo watu wengine bado hawajatambua Unyeti wa Wizara hii, inaniuma sana.

Nafikiri kila mtu anajua ni kwa nini hilo linaniuma saaana, Utamaduni wetu watanzania ni pamoja na mali ya asili ambayo ni Misitu na hifadhi za wanyamapori.

Naumia sana kwa maana Utalii ni pamoja na Wanyamapori, Milima, Maziwa na Mito ambayo ipo hapa Tanzania.

Sasa hebu fikiria kinachonisikitisha zaidi ya yote ni kwamba hata Waheshimiwa Wabunge wenyewe wa Bunge la Jmhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (TANZANIA), hawajui kabisa kuwa Wizara hii ni Nyeti.

Utajuaje kama hawajui kuwa Wizara Nyeti sio Nyeti, ni hivi kwanza Wizara hii haina msaidizi kabisa, Mwanamama
ZAKIA HAMDANI MEGHJI anafanya kazi Mwenyewe kama Waziri wa Malisili na Utalii.

Ni kwamba wabunge walishindwa kushinikiza kuwa Wizara hiyo Nyeti iwe na Msaidizi yaani hapa naamnisha kuwa Wizara hiyo haina naibu waziri.

Mama huyu pamoja na kutokuwa na Naibu Waziri kama ilivyo wizara nyingi tu ambazo zingine zina manaibu Waziri watatu kama ilivyo Wizara ya Fedha anafanya vizur sana.

Angalia Watalii wameongezeka kutoka 295,312 mwaka 1995 hadi kufikia 582,807 mwaka 2004, hii ikiwa ni wastani wa ongezeko la asilimia 10 kwa mwaka.

Hali kadhalika mapato yatokanayo na utalii yameongezeka toka dola za kimarekani milioni 259.4 mwaka 1995 hadi Dola milioni 746.0 mwaka 2004 mabpo mpaka mwaka huo Sekta hiyo ilikuwa imetoa ajira kwa watu wapatao 199,000.

Sasa kwa nini mama huyu ambaye anautangaza utamaduni wa Mtanzania nje ya Tanzania asiwe na Msaidizi? Haya nikisema utasikia ooh wanawake bwana wanataka dezo hatutaki dezo na kazi tuweza sana, Hongera sana Mama Meghji kwa kazi nzuri.

Lakini ni vyema Serikali ya awamu ya nne ikazingatia ushauri huu kuipatia Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii kwa kuwa hii ni Wizara Nyeti kama zilivyo wizara nyingine ikiwezakana atoke Wizara ya Fedha azibe nafasi hiyo.

Angalia utalii wa Tanzania hapa uvayotangazwa bila upendeleo hiyo ikiwa ni kazi ya Mwanamama na mwaka huu anagombea hataki viti maalum tena!!!!!!!

Monday, July 11, 2005

Inapofikia hatua Mtoto Anazaa Mtoto Mwenzie!! What has become of mankind?

Ama kweli sasa tulipofikia ni Karibu na Mwisho, Hivi Yesu atarudi lini? kila mtua ana majibu yake wengine wanasema alisharudi wengine wanasema arudi kufanya nini yote Kheri lakini na tumuombe sana atausaidie kuelewa.

Hii ni picha ya Mtoto mwenye umri wa miaka 10 tu! wa Wilaya ya Kericho Nchini Kenya, kila mtu atauliza sasa kma wa Kericho Nchini Kenya si tufanyaje, Sikiliza ni Mtoto wa miaka 10m ambaye miezi michache iliyopita alikuwa akicheza na wenzie michezo mbalimbali akirudi Nyumbani anaogeshwa lakini sasa amekuwa mama wa Mtoto Jamani tunaenda wapi?!

Kinachoniuma zaidi ni kwamba Baba Mtu mzima ana akili zake ameamua kumfanyia hivi huyu mtoto mdogo ambaye ni sawa na mwanaye wa kumzaa jamani inatia uchungu sana sijui ni wapi tunaelekea Mungu tusaidie kuelewa nini Tunatenda.

Inauma sana, inakatisha tamaa, hebu fikiria mtoto mdogo namna hii anamnyonyesha mtoto mwenzie amezaa anaweza kulea? anaweza kujua iwapo leo mwanangu anaumwa sasa nimpeleke Hospitali? wewe Baba Jitu Zima umemtafutia matatizo ambayo yanamfanya mtoto anaingia katika kitabu cha historia wewe umepumzika.

Ukimuuliza alikuwa anatafuta nini kwa mtoto mdogo tena bado ananuka Shombo kali madai yake mtoto mdogo hana Ukimwi, hatakuwa na ukimwi wakati mizee mizima inataka watoto wadogo?

Na Walaaniwe wote wenye tabia mbaya inayomsababishia mtoto mdogo matatizo katika Siku zote za Maisha yake.
Unakaribishwa kuchangia Bila Jabza wala Upendeleao wa Kijinsia Karibu.

What has become of mankind?

This is a picture of a 10 year old lovely school girl,from the Kericho District in Kenya.
What makes her sospecial? With her whole life ahead of her, a wonderful futureto strive for an education and to move into her teenyears and have fun playing with her fellow girls,children of her own age, she is not playing withdolls.
She is handling the real thing. She has becomea Mother.
Definitely there is a Man somewhere who is to blame!What has become of mankind?People have no fear of the Creator, the Most Merciful,the most Benevolent.
Are we coming to the end?

Tuesday, July 05, 2005

Kwa Nini Sisi Tuweze tuna Nini na Nyie mshindwe mna nini? Mnannisikitisha sana, nyingine mpya hii hapa!!!!!!


NASIKITIKA sana kuona eti asilimia 95 ya Mablogist wa Kiswahili ni Waandishi wa Habari kwa nini lakini?

Mbona mnaifanya mioyo yenu kuwa migumu jamani, Kublog kiwahili sio dhambi, na kama siyo dhami haiwezi kuleta mauti zaidi ya kukupatia faida jamani kwa nini?

kama mnadhani mimi muonugo Fungua Blog nyingine hii hapa www.ngurumo.blogspot.com uone nini kunaendelea.

huyu anaitwa Ansbert Ngurumo ni Mwandishi wa habari Mwandamizi na Nzuri zaidi ni Mhariri wa Gazeti la Tanzania Daima Jumapili, kwa nini basi Madaktari, Maprofesa au hata Wakulima ambao vijiji vyenu vinaendelea mshindwe kuanzisha Blog zenu jama?

wala haihitaji fedha kwa ajili kuanzisha na kumiliki Blog, nawaombeni jamani Bogo si kwa ajili ya Waandishi wa habari ni kwa yeyote Mwenye nia ya kumiliki. msiogope jamani tafadhali msiogope.

Sunday, July 03, 2005

Junior naye Eti anasikiliza Nyeti ya Wagosi


WATOTO ni rika moja ambalo asipolelewa vyema basi ama atafanya maajabu ama madudu katika ulimwengu huu.

lakini pia utandawazi unaharibu sana watoto katika ulimwengu huu ambao wataalam wanauita ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia.

Sasa Hebu angalia Junior anasilikiza Music naelewa kweli halafu mziki wenyewe wa Wagosi wa Kaya, unaitwa 'NYETI'.

HIVI KWELI TUTAFIKA JAMANI?