Friday, October 28, 2005

AKIFA Mwingine uchaguzi si utafanyika 2006? Mrema naye Hoi kitandani!

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), jana imetangaza kuahirishwa kwa uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani kufuatia kifo cha aliyekuwa Mgombea urais Mwenza wa CHADEMA kufariki dunia.

NEC imetangaza tarehe mpya ya uchaguzi kuwa nui Desemba 18 mwaka huu kuanzia saa 1.00 asubuhi hadi saa 10.00 jioni.

nilipopata tarifa hizo jana nilishtuka sana kwa maana kwanza huyo mgombea mwenyewe ukweli nilikuwa simfahamu kabisa kwa jina wala kwa sura, ushanipata bwana?

unajua kitu gani kimenishtua ni hiki: uchaguzi umeahirishwa hadi Desemba 18 mwaka huu, eti mpaka CHADEMA wateue mgombea mwenza mwingine wamnadi halafu ndo watu wampigie kura!

unajua inachekesha sana, panapochekesha ni hapa: huyo marehemu mwenyewe ni watu wangapi walikuwa wanamfahamu? na je huyo atakayeteuliwa atapa kura ngapi?

haya muda nao sasa akifa mwingine itakuwaje? maana mrema naye ambaye ni Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama cha TLP ni mgonjwa hoi bin taaban kitandani! kwa kweli tume imenichanganya sana.

kwanza wagombea wenyewe wamechoka na kampeni, lakini pia hata sisi wananchi pia tumechoka, cha msingi sasa ni mara bunge litakapopatikana itabidi libadilishe sheria zote zilizopitwa na wakati ikiwemo hii sheria ya uchaguzi ya mwaka 1985 maana imenichefua sana.

zisiporekebishwa Serikali yenyewe itajikuta siku moja inajifunga na sheria iliyotunga yenyewe na mbaya zaidi mpaka sasa jumla ya sh. bilioni 43 zimeshatumika kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi, ambapo jumla ya sh. bilioni 93 zimetengwa kwa ajili ya uchaguzi huo ambao sasa utafanyika Desemba 18.

Mimi nimechoka sana na siasa za inji hii sijui nyie wenzangu mnazionaje?

Thursday, October 13, 2005

Kha! Kumbe Nchi Imeshaposwa? Wenye Nchi tunafanyiwa Kicten Party Sasa!!

HAKI ya Mungu sasa Tanzania tunakoelekea kubaya sasa, Ni jana tu nilikuwa nasoma Blog ya Bw. Msangi nikakutana maoni ya Watu wengi sana kuhusiana na Matunda ya Uhuru ambaye kwa sasa yamegeuzwa Matundu ya Uhuru!

kilichonishtua zaidi baada ya kusoma maoni ya msomaji mmoja ambaye alisema kwa sasa Tanzania imeshatolewa Posa na Wawekezaji toka nje ya Nchi ambao kabla ya kuioa Tanzania bado wanaifanyia Kitchen Party!

Mbaya zaidi waowaji hao wanakuja na mashartimagumu sana kwa waolewaji jambo ambalo linawakandamiza sana waolewaji lakini cha kujiuliza ni hiki je ni Kweli Tanzania haina uwezo wa kutafuta vitendea kazi vyenye ubora wa kimataifa na kufanya kazi zake yenyewe na kuwauzia haoa hao wanajiita wawekezaji?

Najisikia hasira sana ninapoona Mkurugenzi wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita ni Mzungu wakati kuna watanzania ambao wana uwezo wa kufanya kazi hiyo ya Ukurugenzi katika Mgodi kama huo.

Sasa sisi watanzania ambao tunafanywa Mali Ghafi tufanye nini ili Tusikandamizwe na hawa waowaji wenye masharti Makali namna hii?