Saturday, December 10, 2005

Hii ndio Hali halisi ya Wabongo!!!!!





HII ndio hali halisi ambayo inatukuta wabongo wengi hapa kwetu, kagari kadogooo lakini watu kibao, utadhani marobota ya Pamba yanasafirishwa toka shinyanga kwenda Dar es salaam kwenye kiwanda cha kutengenezea Nguo.

halafu mbaya zaidi gari hii ikakosa mafuta na kuna watu wana haraka zao wengine wagonjwa, wengine wanawahi Benki kuchukua hela kwa ajili ya kununulia mahitaji yao na mbaya zaidi siku yenyewe ni ya Jumamosi ambayo ni nusu siku!

safari moja huanzisha nyingine, yalishamkuta Mgombea urais Mwanamke Pekee , Komando Anna Senkoro mara Wese si likamuishia!!!!!!!!!!!!!!!!! basi bwana akaanza kuchangisha fedha kwa ajili ya kununua Mafuta kama CHAMA CHA MADAKTARI WANAWAKE (MEWATA), wanavyoomba kuchangiwa fedha kwa ajili ya uchunguzi wa saratani ya matiti kwa akina mama!

sasa mbaya zaidi ni kwamba pamoja na gari hili kujaza watu kibao babaake! sheli hakuna wese wala nini ili kuepuka usumbufu kwa wafanyakazi kuulizwa mafuta yapo? wameamua kuweka Bango Kubwaaaaaaaaa, Eti NO FUEL! UNGEKUWA WEWE NI MMOJA WA ABIRIA KATIKA GARI HII UNGEFANYAJE?

Nakaribisha maoni, changia bila jazba wala upendeleo!