Monday, October 09, 2006

Tuesday, August 01, 2006

Kama Mnabisha muulizeni Michuzi!!!!

WELCOME!!!!!
Nikikwwambieni Wasomaji wangu niko Bize naomba muamini na kama hamuamini mumuulize Michuzi, ilibidi tu tuipige ili kuthibitisha kauli yangu niiyoitia kijiweni, hapa ni katika viwanja vya Bunge, Blogaz. (Michuzi kushoto na Martha D. M).

Monday, June 12, 2006

HAPA NI MHESHIMIWA MBUNGE NDO KAVAA HIVI JE ALIPOKUWA PAPARAZI KAMA MIMI ILIKUWAJE?????!!!!!!!!


MHISHIMIWA AMINA CHIFUPA MPAKANJIA(CCM)!!!!!!!
HAKI YA NANI, INASEMEKANA MBUNGE HUYU NDIYE ANAYEONGOZA KWA KUJIRUSHA KULIKO WABUNGE WENGINE AKIFUATIWA NA BIBIE HALIMA MDEE MBUNGE WA VITI MAALUM (CHADEMA). MBUNGE MWANAUME ANAYEPENDA KUJIRUSHA NA MWENYE UMRI MDOGO KULIKO WENGINE BADO SIJAMPATA KAMA KUNA MTU ANAFUNUNU HIZO BASI ANITONYE!

Tuesday, May 02, 2006

Uhuru wa Vyombo vya habari Tanzania Bado ni Ndoto.

Kila mwaka Mei 03 Wanaharakati kote ulimwenguni husherehekea Siku ya uhuru wa Vyombo ya habari Duniani Swali ni Je uhuru huu hapa Tanzania upo au bado longolongo? jadili bila jazba wala upendeleo karibu!!!!!!!!!!!

hivi ndivyo mzee wa sumo na mwenzie walivyoumizwa na askari magereza walipoenda kukava raia wanavyoondolewa kwa nguvu kwenye nyumba zilizokuwa za atc na kununuliwa na magereza kule ukonga. kesi iko inanguruma mahakamani kwani askari jela waliohusika walishtakiwa. Picha na Issa (Michuzi)

Monday, April 03, 2006

Amini! Gari ya hakimu iliyoibwa yapatikana!

Gari ya hakimu iliyoibiwaimepatikana eneo la Yombo Buza wilayani Temeke. Gari hilo limepatikana likiwa limeng'olewa Vipuri mbalimbali ikiwemo vyenye thamani ya sh. milioni 1.1.

Hakimu safari alisema kutokana na gari hilo kutokuwa na mafuta ya kutosha ndio sababu iliyowafanya wezi hao kuliacha gari hilo baada ya kuishiwa mafuta. Gari hilo linashikiliwa katika kituo cha polisi Chang'ombe na Polisi bado wanaendelea kuwasaka walioiba gari hilo!!!!!!!!! haya mnasemaje?????

Wednesday, March 29, 2006

HAKI ya nani, yaani kweli wabongo sasa tumedata, hebu soma hii kwa makini halafu ufikirie itakuwaje! HAKIMU Mkazi wa Kisutu Jijini Dar Es Salaam juzi Mahakamani aliibiwa gari lake aina ya Suzuki Samurai wakaiti akiendesha Kesi.

Gari hiyo lina thamani ya sh. Milioni 3.5 na aliibiwa akiwa Bize na Masuala ya Kesi Mahakamani hapo.

Hakimu Safari aliibiwa gari hiyo yenye namba za usajili T867 ALA, ambali inadaiwa liliibiwa saa nne asubuhi baada ya hakimu huyo kufika katika eneo lake la kazi na kuegesha.

Baada ya kumaliza shughuli zake za kikazi mahakamani hapo hakimu huyo alitoka nje ya jengo la mahakama akiwa na funguo za gari hilo kwa nia ya kurejea nyumbani na ndipo alipogundua kuibiwa kwa gari hilo.

hakimu huyo alisema kazi kulitafuta gari lake limo mikononi mwa polisi baada ya kuropoti kwa mkuu wa makosa ya jinai (RCO), gODFREY nZOWA ambapo alipatiwa RB namba CD/RB/3147/06.

HII NI KALI KULIKO YA MWANDOSYA AMBAYE ALIVAMIWA KIWA BAA HIVI ALIYEIBA GARI HIYO AKIKAMATWA NA KUFIKISHWA MAHAKAMNI HAPO KWA HAKIMU HUYO ALIYEIBIWA GARI YAKE ANAWEZA AKAPEWA ADHABU GANI???!!!!! INATISHA.

Tuesday, January 31, 2006

Kweli Mjuu hamnazo! Waziri Mkuu atangaza kuacha ngono hadi uchaguzi umalizike!!!!

ukishangaa ya Musa utastaajabu ya Silvio Berluscon, haki ya mungu !Waziri Mkuu wa Italia Bw. Silvio Berlusconi amewashangaza walimwengu baada ya kutangaza kuacha ngono hadi Aprili 09 mwaka huu baada ya uchaguzi wa inji hiyo kumalizika.

unajua nini mpenzi msomaji huyu sio kama hana akili ila ametoa changamoto kwa viongozi wote ulimwenguni kuwa serious na mambo magumu na hasa katika wakati mgumu wa uchaguzi kuacha kabisa masuala ya NGONO, ili kujua nini kinaendelea na kama huamini soma habari hii kwa lugha ya kisasa hapa chini.


Berlusconi 'in pre-poll sex ban'

Italian Prime Minister Silvio Berlusconi has surprised followers with an unusual pledge - to give up sex until after April's general election.

Mr Berlusconi, 69, reportedly made the vow at a campaign rally in Sardinia with a popular local TV preacher.

Father Massimiliano Pusceddu had praised him for opposing gay marriage and defending family values.

In remarks quoted by Il Giornale newspaper, Fr Pusceddu promised his support, prompting the PM's comments.

"I will try to meet your expectations, and I promise from now on, two-and-a-half months of absolute sexual abstinence, until 9 April," he said.

Jokes

Mr Berlusconi has been criticised in the past for using sexual innuendo and making sexist jokes.
Last June, the prime minister stunned the Finnish government by saying he had used his "playboy" charms to persuade female President Tarja Halonen to give up attempts to house the EU food agency in Helsinki.

And in 2003 he told US business leaders they should invest in Italy because it had "beautiful secretaries... superb girls".

Correspondents say the twice-married Italian leader sees himself as something of a ladies' man.

He left his first wife 27 years ago to marry glamorous blonde actress Veronica Lario, but there have been rumours in recent years of marital problems.

Ends.....

Thursday, January 26, 2006

KWA STYLE HII, WABONGO MWAKA HUU TWAFA



Hii ndio hali ya Bongo kwa hivi sasa, hakuna pesa hakuna mvua wala hakuna biashara inayofanyika zaidi ya biashara kujiozea na wauzaji kupumzika kwa staili hii ambapo ataamshwa na njaa kali ambapo atakuwa anahitaji menu hiyo hapo kulia, wakati mfukoni hana hata shilingi, jamani tufanye nini wenzenu twafa! tena twafa vibaya maana tutakufa bila ubishi, israeli atatukuta tumepumzika hii ikiwa na maana kuwa tutakufa bila kuugua wala kupata ajali, Ndugu zanguni tumwombe sana mungu atusaidie!!! (picha kwa hisani ya Issa Michuzi)