Wednesday, March 29, 2006

HAKI ya nani, yaani kweli wabongo sasa tumedata, hebu soma hii kwa makini halafu ufikirie itakuwaje! HAKIMU Mkazi wa Kisutu Jijini Dar Es Salaam juzi Mahakamani aliibiwa gari lake aina ya Suzuki Samurai wakaiti akiendesha Kesi.

Gari hiyo lina thamani ya sh. Milioni 3.5 na aliibiwa akiwa Bize na Masuala ya Kesi Mahakamani hapo.

Hakimu Safari aliibiwa gari hiyo yenye namba za usajili T867 ALA, ambali inadaiwa liliibiwa saa nne asubuhi baada ya hakimu huyo kufika katika eneo lake la kazi na kuegesha.

Baada ya kumaliza shughuli zake za kikazi mahakamani hapo hakimu huyo alitoka nje ya jengo la mahakama akiwa na funguo za gari hilo kwa nia ya kurejea nyumbani na ndipo alipogundua kuibiwa kwa gari hilo.

hakimu huyo alisema kazi kulitafuta gari lake limo mikononi mwa polisi baada ya kuropoti kwa mkuu wa makosa ya jinai (RCO), gODFREY nZOWA ambapo alipatiwa RB namba CD/RB/3147/06.

HII NI KALI KULIKO YA MWANDOSYA AMBAYE ALIVAMIWA KIWA BAA HIVI ALIYEIBA GARI HIYO AKIKAMATWA NA KUFIKISHWA MAHAKAMNI HAPO KWA HAKIMU HUYO ALIYEIBIWA GARI YAKE ANAWEZA AKAPEWA ADHABU GANI???!!!!! INATISHA.