Thursday, October 18, 2007

ALBADIR dhidi ya UbaBE BuNgeNI!!

Baada ya ubabe ndani ya Bunge na kumuondoa Bwana Zitto Bungeni na Bunge kuvunjwa wale wote walio msakama na kumfanyia nyodo wamesha kutwa na haya yafuatayo;

Kwanza alianza Ruth Msafiri wa Muleba Kaskazini. Mumewe alipata ajali mbaya ya pikipiki na kukimbizwa Muhimbili na alifia hapo Mhuhimbili lakini haikutangazwa .

Baadaye Peter Selukamba akiwa anaendesha mwenyewe alinusurika kifo baada ya gari lake kuwa kama chapati yaani ile VX yake ya Ubunge na hadi sasa gari halitamaniki lakini akapona kuumia . Hawakuandika kokote wakafanya siri.

Siku hiyo hiyo Mbunge Malima akiwa anaendesha yeye mwenyewe akapata ajali pale uwanja wa JK Nyerere akanusurika kuumia lakini gari inahitaji matengenezo makubwa waandishi wa majira kimya hawajasema lolote . Baadaye akaja Mudhihiri wote mnayajua ya kwake.
Juzi kapata ajali mbaya sana ndugu Kumchaya Selemani wa Lulindi.Watu 2 wamekufa na yeye kanusurika .

We all have also heard about Juma Kapuya ……

Je hiki ni kitu gani ? Mungu kutupigania Watanzania ?

Je kwa nini vyombo vya habari visiandike? Au Albadir ilyosomwa na watu wa mwisho wa reli si mchezo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Jamani waheshimiwa kuweni makini wakati wa kuongea maisha haya huwa mafupi pale yanapoanza kuwa matamu!