Wednesday, April 02, 2008

JAMANI Sikujua kama ndugu zangu Wagogo tuna uchungu na mifugo namna hii!!! hebu soma hii halafu unipe jibu!!1

MFUGAJI mmoja amekufa baada ya kunywa sumu aina ya Daimeko baada ya kukuta mkewe na mfanyakazi wake wakiwapiga ng’ombe wake.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa Michael Kamhanda aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa Mfugaji huyo Philemoni Mkunaa (35), alikunywa sumu hiyo baada ya kuona kuwa ng’ombe wake wanateswa.

Akielezea tukio hilo Kamhanda alisema kuwa siku ya tukio majira ya saa tisa usiku aktika kijiji cha Lamiti tarafa ya Mundemu wilayani Bahi, akitoka katika pombe Mkunaa alimkuta mkewe na mchungaji wake wa ng’ombe wakiwapiga ng’ombe hao ambapo aliwauliza kwa nini wanawapiga ng’ombe na kujibiwa kuwa wanawapiga ili waingie zizini.

Alisema kuwa baada ya kupewa jibu hilo mfugaji huyo alisema kuwa hawaoni kama wanavyowapiga ng’ombe hao wanawatesa na kama wanawatesa ng’ombe hao yeye atakuwa sumu ili afe.

Kamhanda alisema kuwa baada ya kuona bado ng’ombe wake wanapigwa Mkunaa aliingia ndani na kuchukua dawa aina ya Daimeko na kunywa na baada ya muda alianguka na kufariki.

Katika tukio lingine Jeshi la polisi linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kumpiga fimbo na kumuua mtu mmoja aliyejulika kwa jina la Yohana Chiloleti (16), mkazi wa kitongoji cha Makeweni wilayani Kongwa.

Kaimu kamanda Kamhanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira saa moja jioni baada ya Chiloleti kuchungia ng’ombe karibu na nyuma ya watuhumiwa hao.

Kamhanda alisema kuwa baada ya watuhumiwa hao kuona chiloleti akichungia ng’ombe karibu na nyumbani kwao walimhoji nkwa nini anachungia hapo na ndipo alipowajibu kuwa kwani kuna tatizo gani ndipo watuhumiwa hao walianza kumshambulia kwa kumpiga na fimbo kichwani hadi kufa.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Sisemi Mgoya (15), na Semarungo Mgoya (17), ambapo wanatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.

Ends………..