Wednesday, June 23, 2010

Et ni kweli kwamba kumkeketa Mtoto wa Kike kunamfanya asiwe Malaya?

HIVI ni Kweli eti kumkeketa mtoto wa kike ni kumfanya asiwe Malaya jamani? Ninauliza hivi nina maana, moja ya mila na tamaduni za wagogo hapo zamani ilikuwa ni kumkeketa motto wa kike ili kumfanya asiwe Malaya.

UNAOBA bwana, unajua kwa nini? Eti wabibi wale wa zamani wanasema kuwa ukimekeketa mtoto wa kike unampunguzia hamu ya kufanya mapenzi na hivyo anakuwa si Malaya!
Sasa sina uhakika kama ni kweli sana, naomba wadau mnisaidie katika hili tafadhali naombeni jamani, naomba mtoe maoni yenu halafu baadaye nitafunga mjadala kwa kuwa bado natafuta materials zaidi ya kuwafahamisha kuhusu mila hii ya mgogo!

Karibuni sana.