Saturday, August 20, 2005

Nikusikie tena unatishia watu Amani!


Inasemekana Vyama vya upinzani vinafanya fujo makusudi kutokana na wagombea wa Vyama hivyo kujua kuwa havitashinda katika uchaguzi Mkuu ujao.

Lakini kwa mujibu wa Wachunguzi wa masuala ya Siasa wanasema kuwa ni katika kujitetea tu ndio maana vyama hivyo vinafanya hivyo,

Je wewe Msomaji wa Blog hii una maoni gani? unafikiri ni kwa nini inakuwa hivyo? weka maoni yaklo hapa ili unisaidie kuelewa ni kitu gani kifanyika na kwa malengo hani hasa, unakaribishwa kuweka hoja zako bila jaza wala upendeleo wa aina yoyote.

Karibuni.

Tuesday, August 16, 2005

Ni kama anasema "Ndejembi Mwenzio najisikia Kizunguzungu nisaidie ninyanyuke hapa nisije nikaanguka!" Huyu Makamu Mwenyekiti wa CCM na Muasisi wa CCM Mzee Rashid Mfaume Kawawa ambaye jana alishindwa kuendelea kuhudhuria Mkutano Mkuu wa CCM almaarufu NEC kutokana na kuugua ghafla akiwa ukumbini. Mzee tunalkubali mchango wako saaana lakini pumzika sasa umechoka he! unataka kufa kishujaa?
Kwa habari zaidi Soma hapa.

Wednesday, August 03, 2005

HAYA TENA MABLOGST WANAZIDI KUONGEZEKA!!!!!

Ni waandishi wa Habari tu tena toka Dodoma, huyu nae ni Mpiga Picha wa ITV Dodoma naitwa Twaha kivale, Bonyeza hapa umsome.

Tuesday, August 02, 2005

Si Ulitaka Chai! Iweje ulalamike Unaungua?



Baada

Haya Jamani tukiambiwa tuache kunywa Chai kavu tunang'ang'ania Tu na Matokeo yake ndo haya Tunaungua, Kunywa chai na Vitafunio hata ikiwa ya Moto Kiasi gani huwezi Kuungua kama ilivyomuunguza marehemu Mrembo Huyo ambaye alikuwa akisoma Chuo Kikuu cha MOI huko Nchini Kenya.

Alipojijua kama ameambukizwa Virusi ya Ukimwi akaahidi Kulipiza Kisasi kwa yeyote ambaye atakatiza Machoni Mwake na alifanikiwa kuambukiza Jumla ya Wanaume 124 nchini humo ambao waliopona ni 6 kwa kuwa walimua kunywa chai na Vitafunio.

Kabla alikuwa Mrembo sana kama anvyoonekana katika Picha ya Chini
Nawaombeni sana Radhi Wapenzi wasomaji wa Blog yangu, kwa kuchapisha Picha ya Kutisha namna hii hii inasababishwa na Mimi kuguswa sana na Tukio hili.
Kunyweni Chai na Vitafunio Jamani la Sivyo Tutaungua!