Monday, October 06, 2014
Hivi ndivyo wagogo wanavyowazika waliokufa kwa kifafa!!!
Wednesday, August 31, 2011
habari njema kwa wenye vitambi na mafuta mengi mwilini
Wednesday, March 30, 2011
Monday, August 02, 2010
Wednesday, June 23, 2010
Et ni kweli kwamba kumkeketa Mtoto wa Kike kunamfanya asiwe Malaya?
UNAOBA bwana, unajua kwa nini? Eti wabibi wale wa zamani wanasema kuwa ukimekeketa mtoto wa kike unampunguzia hamu ya kufanya mapenzi na hivyo anakuwa si Malaya!
Sasa sina uhakika kama ni kweli sana, naomba wadau mnisaidie katika hili tafadhali naombeni jamani, naomba mtoe maoni yenu halafu baadaye nitafunga mjadala kwa kuwa bado natafuta materials zaidi ya kuwafahamisha kuhusu mila hii ya mgogo!
Karibuni sana.
Friday, March 05, 2010
HIZI NI SALAMAU ZA WAGOGO KUTOKA KWA KAKA FREDIRICK MUMBULI!
Nimefurahi kuona kazi nzuri unayoifanaya, ni Tuvuti nzuri ikieendelezwa na ikapata habari nyingi moto moto.
Kumekuwa na jitihada nyingi kukujaribu kuwakumbusha na kuwahamasisha Wagogo kuungana na kufanya kazi za maendeleo na hususani za kiuchumi (Ujasiriamali) lakini nyingi ziko kwa mwendo wa kinyonga, Wanyausi wamebaki na kilio cha Ukame (Chibahu) na umasikini!
Leo hii ukijitambulkisha mgogo haraka kwenye mawazo ya “wanyamunthu” kunakuja wazo la omba omba/masikini, siku hizi tumewafunika hata watani zetu, maana sisi tuna hata mbwembwe za aina aina za kuomba! Lakini kwa nini, au kuna nini vichwani mwa wanyausu?
Kwa nini tusizinduke sasa, mbona wakati tulalamika ukame na umasiki uliokithiri, shemeji zetu Wachaga wanaporomosha majumba ya magari ya kifahari, kwani hivi wanavuchumia wapi! Mbona waheshimiwa kutoka kondoa wanachangamikia tenda, sisi tumebaki “usiku wo monga!”. Haya sasa Vyuo hivyo, wanakuja watoto wa wenzetu wanapata elimu wanarudi kutumikia makwao, hata kama kuna wazalendo wanachuma wanaenda kujenga kwao na baadhi wanawekeza Dodoma.
Wanyausi wana nini, mbona wapo kama wameridhika tu na maisha duni! Tumesikia madinai yalipatikana maeneo Fulani huko Mpwawa wamekuja wenzetu wajanja wakachota, hata huko Wilaya mpya kunatetesi chini kuna mali, badala ya kushiriki midahalo na mijadala mbalimbali nasikiwa wanyausi wameshafyata mkia wao wanafikilia Matembe yao wataenda kuyaotesha wapi!
Wanyausi, Zabibu! Wataliano huko Homboro wanabweda tu, hebu jaribu kuulizia Mvinyo wa Homboro kama utaupata kwa urahisi hapa nchini labla uende majuu Hongera Wanyausi wa Chinangali kuanzisha tena zao la zabibu, lakini angalieni isiewe nguvu ya soda! Kwani hamkumbuki enze za zabibu Mlowa bwani, Kigwe na kungineko vijiji vilinunua mpaka Malori, magari na mashamba hayo vikowapi.
Hongera ndugu zangu wa Mbabala! Kumbe tukiwezeshwa tunaweza, sasa hebu CRDB iingalie na Miradi mingine, kama Ubuyu, unashanga! Hebu tukikusanya maauzo yote ya ubuyu Dalisama tu, mboana watu wanalipa kodi na ada za shule” nkani ya mapela” Mazao kama Alizeti, ufuta na karanga yakiwezeshwa, mashudu tutalisha ng’ombe, na mbuzi wataongezeka mnadani.
Wanyausi, sasa tena hata Nindo, Msunyunto, Muheme, Chipande, Masembegu Chiganda, taja…… hatuvisamini tena, si hata tungetengeneza Single na sisi tukatoka Maanderground! Mbona inawezekana, mbona Dada yetu kavaa koti ya Chimuli akatoka naye alitoka Tanga.
Kaka zangu Mavunde na Yobwa, papa Mchoya yuko wapi? Najua kazi nzuri za huko St. James Arusha, UVUKE-DodoMA, taja.............. Mvua hainyeshi, mbona kumeanzishwa kiwanda cha maji, Sante! Kwani maji ya mzakwe yameisha, mto Bubu vipi sikuizi unaongea, hayo maji tuyafate huko huko chini, Hiviiiiiiii mbona Waarabu hawahami jangwani, sisi kila siku mabasi kwa basi DALISALAMA, tunawaachia wenzetu nyumba, mnategemea nini!
Si ajabu waheshimiwa hawataki kuhamia Dodoma maana wanashanga nyie mnawambia wahamie Dodoma, lakini mnapishana nao Dumila, mkienda Dalisalama, nyinyi mnakimbia nini, halafu mnawazimisha wahamie Dodoma, hiviiiiiii mmesahau usemi wa Wanyausi “Mnyanyumba sangalale……..” Y ako mengi yakusema, lakini iko haja ya wanyausi kufikiria tena, Dodoma tunamwachia nani, Mzee mkubwa, Baba, Koko wewe tu umebaki kati ya Wazee wetu, hivi mkikaa na Mzee mwenzio hamweza kutuamusha, mwene chibede cha chichi! So chi wayangu! Sema neno moja tu mbona tunakuaminia.
Sasa hebu angalia wageni wanakuja sisi tunatoka kwenye vibarua Dalisalama, hata kweli ni adamu ya “KWI KUMBU” tuliojifunzo, ng’o yai! George Kusila alinza kitu cha Wanyausi kuwakumbusha walikotoka, basi hata wakishindwa mengine, miili tu irudishwe ikazikwe kijijini, hata hilo nalo limekuwa gumu, hiviiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii! Kalumbu asante sana, kwa wasaa huu naomba nikukaribishe kikao cha wanyausi 14/02/2010 Dalisalama , tunapanga sehemu ya kukutana ukinipigia baada ya kesho nitakuwa na jibu.
Wakutya Wagogo chili Chibede, chili machela vitatufikisha wapi ndugu zanguni! Salaam.
from Freddy Kapande (Kigwe) mumbuli@yahoo.com 0715327683
Monday, January 04, 2010
HAPPY NEW YEAR 2010
Nakutakieni heri ya mwaka mpya wa 2010 wasomaji wangu wooote hata wale ambao huwa munapita tu angalau kwa mara chache saaana, nawashukuru sana wote ambao mmekuwa mkitoa ushauri wenu na mawazo mbalimbali na kuifanya webpage hii kuendelea kuishi katika ulimwengu huu wa Utandawazi! Thank U sana all of u! be blessed Oh!
Thursday, November 26, 2009
TANZIA!
Nawashukuru sana wote waliojitolea kwa hali na mali kumsaidia mariam ili aweze kutibiwa, ndugu zangu waliomsaidia mariam HINAI TAMIM na SAID wote wa nchini Oman Muscat, mungu awazidishie baraka muendelee na moyo huo.
Mungu ailaze mahali Pema Peponi roho ya Mariam Obed
AMEN!!
Monday, November 09, 2009
Monday, September 21, 2009
MAPENZI hayana umri jamani, hebu msome mzee wa miaka 70 aliyejinyonga kwa wivu wa mapenzi!
9/21/2009
MZEE wa miaka 70 aliyefahamika kwa jina la Msuliche Mhogo amejinyonga kwa kutumia kamba kutokana na wivu wa mapenzi.
Kamnda wa polisi mkoani hapa Zelothe Steven aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 2.30 asubuhi katika kijiji cha Ngh’ambi wilayani Mpwapwa.
Akielezea tukio hilo Kamanda Zelothe alisema kuwa chanzo cha mzee huyo kujinyonga ni kutokana na wivu wa kimapenzi kwa mkewe mwenye umri wa miaka (30) ambaye jina lake limehifadhiwa.
Alifafanua kuwa kwa muda mrefu mzee huyo alikuwa akihisi mkewe ana uhusiano wa kimapenzi na mwanaume mwingine hapo kijijini ambaye ni jirani yake.
Alisema kuwa awali kabla ya tukio hilo kutokea , usiku mzee huyo aligombana na mkewe kuhusu mtoto wao mmoja ambaye ana umri wa miaka miwili akidai kuwa mtoto huyo ni wa mwanaume ambaye nahisi anatembea naye na si mwanaye.
Kamanda Zelothe alisema kuwa wakati wakiendelea na ugomvi huo mke mkubwa wa mzee huyo alienda kuamua ugomvi huo na ilipofika asubuhi mzee huyo aliaga kuwa anaenda safari na ndipo alipokwenda kwenye mbuyu ambao upo jirani na nyumbani kwake na kujinyonga.
Wakati huohuo jeshi la polisi mkoani hapa linamshikilia Hamis Salum (27) mkazi wa Manispaa ya Moshi kwa tuhuma za kufungua duka na kuiba simu 10 za aina mbalimbali.
Kamanda Zelothe alisema kuwa baada ya kufungua mlango mtuhumiwa huyo alijfungia ndani ya duka hilo na kuanza kukusanya simu dukani humo ambapo mwenye duka ambaye ni Freeman Narcis (23) alifika dukani hapo na alipofungua duka alimkuta mtuhumiwa huyo akiendelea kukusanya vitu katika duka hilo .
Kamanda Zelothe alisema kuwa jeshi hilo bado linamshikilia mtu huyo kwa mahojiano zaidi na atafikishwa mahakamni mara baada ya uchunguzi kukamilika.
Ends……
Thursday, August 20, 2009
Ningekuwa Spika Sitta Ningejiuzulu!
HAKI ya Mungu kweli duniani kuna mambo pamoja na mambo yote mazuri ambayo spika wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania Samuel Sitta kwa Wabunge wa chama cha mapinduzi wakiwemo na Mafisadi ambao wanajulikana kwa majina mimi sitaki kuwataja bado wabunge hao ambao wengine ni wajumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (NEC) na mafisadi wamo wamememgeuka!
Jamani kwa kweli ni lazima tukajifunza ustaarabu mengi sita kawasaidia wabunge hawa pamoja na wale wa upinzani lakini sasa tena moto umemgeukia yeye jamani kweli hii ni fair?
Hapa naorodhesha tu mambo machache ambayo spika sitta amewapigania wabunge hawa na kubalansi Bunge ili liliemee upande mmoja halafu akaonekana kana kwamba anapendelea upande mmoja wa CCM!
Spika huyuhuyu ambaye anaitwa Mbabe amepigania kwa nguvu marupurupu ya wabunge na kusababisha sasa hivi wabunge kulipwa mshahara tu kiasi cha sh. Milioni 12 kwa mwezi na marupurupu kibao!
Hiyo haikutosha spika huyohuyo mbabe amepigania mpaka sheria ya kuanzishwa mfuko wa maendeleo ya Jimbo kwa wabunge umepita kwa mbinde Bungeni licha ya wananchi kuonyesha kuukataa!
Mimi sijatumwa na Mtu kuzungumzia hili suala ila nimeguswa na kitendo alichofanyiwa hivi karibuni Mjini Dodoma katika Ukumbi wa Nec wa kutaka avuliwe uanachama kwa kuwa anaendesha eti Bunge kibabe!
Kwa kweli CCM hamkumfanyia Spika wenu sawa kabisa kwa sababu mnataka aliendesheje Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambalo hivi sasa limekuwa kama Kikundi cha vichekesho cha orijino Komedi kuna jambo lingine zaidi ya hili si mseme?
Alichokisema hivi karibuni Bungeni spika kuwa anaomba ulinzi wa ziada kwa kuwa nguvu ya mafisadi inamzidi alikuwa sahihi kwa kuwa tayati alishaona nini kinafuata na kwa kuwa serikali haikumuelewa ndiyo maana ilipuuzia na maneno meengi ya kejeli yakatolewa juu ya kauli yake!
Lakini ukweli wa maneno ya Mzee Sitta sasa yamejidhihirisha ndani ya mkutano wa CCM ambamo kunaonekana kuwa CCM bila mafisadi haiwezekani kuwa hai, sasa mnataka spika aendesheje Bunge lenu JAMANI?
Mnataka spika atoe uhai wake ndiyo mbaini kuwa alikuwa anaendesha bunge kwa usawa na kubalansi pia au mnatakaje au aendeshe Bunge kwa kupendelea wabunge wa CCM? Mtalishusha hadhi na viwango pia kama mnataka liwe ambavyo ninyi mnataka liwe!
Kwa kweli inauma halafu inakera zaidi inatia kichefuchefu kufanya hivyo ni kuonyesha ni kiasi gani kwamba CCM inashikiliwa na kuendeshwa na watu wachache wenye pesa zao na utartibu huu ambao CCM mmeuonyesha sijui nini kitafuata lakini mmetia DOA tena doa lenyewe jekundu kwenye nguo nyeupe!
SHAURI YENU CCM angalieni msije mkajuta kwa kuwasafisha watu ambao tayari walishachafuka siku nyingi kupitia watu ambao wangekusaidieni kuwasafisha angalau kwa kutumia busara zao ambazo zinaonekana ni ubabe!
Tuesday, June 23, 2009
Wasamalia wema wamsaidia Binti Mariam


Tuesday, May 05, 2009
WENZETU HUKO TARIME wanadumisha mila kwa mtindo huu
hebu soma hii kwanza.
Katika mkoa wa Mara kuna mila ambayo imekuwa ikifanywa na wazee wa kimila ambao kutokana na kutekeleza mila hizo matukio ya mauaji yamekuwa yakisababishwa na mapigano ya koo mbalimbali.
Mila hiyo imesababisha hali ya ulinzi na usalama mkoa ni mara kutokuwa shwari na kutoridhisha kutokana na matukio ya mara kwa mara ya mauaji ya kiukoo, wizi wa mifugo, ujambazi wa kutumia silaha na biashara ya madawa ya kuelevya hususan kilimo cha Bangi.
Wazee wa Kimila Mkoani Mara ndiyo viongozi na waamrishaji wa mapigano ya koo yanayondelea, ambapo wazee hao hunufaika na mapigano hayo kwa kupata mgao wa mali zilizoporwa katika mapigano.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrance Masha anasema kuwa mila na desturi za baadhi ya makabila zinachochechea mapigano baina ya vijana wa koo moja na koo nyingine vitendo ambavyo vimekuwa vikiheshimika miongoni mwa jamii hizo kuwa ni vya kishujaa.
Waziri Masha anasema kuwa wazee wa kimila wamekuwa viongozi na waamrishaji wa mapiganmo hayo ambapo wamekuwa na maradaka makubwa katika Koo zao na hutoa adhabu kali kwa vijana wanaokwepa kushiriki mapigano.
Waziri Masha anasema kuwa kutokana na hilo, hadi sasa hali ya ulinzi na usalama katika mkoa wa Mara si ya kuridhisha kwa kuwa kumekuwa na matukio ya mara kwa mara ya mauaji ya kiukoo, wizi wa mifugo, ujambazi wa kutumia silaha na biashara ya madawa ya kulevya hususan kilimo cha bangi.
Anasema kuwa matukio hayo yameenea katika wilaya za Tarime, Rorya na wilaya ya Musoma vijijini ambapo koo za hunyaga na Wamera na koo za Waanchari na Warenchoka na Wakira na Wanyabasi na Wairegi zimekuwa zikipigana mara kwa mara.
Masha anasema kuwa kilimo cha Bangi ambacho kimekuwa ni chanzo kikubwa cha uchumi kwa baadhi ya makabila katika mkoa wa Mara, pia kimekuwa ni chanzo cha mapigano hayo ambapo imekuwa ni kawaida kwa watu katika maeneo hayo kukodishwa na wakala kulima bangi na kulipwa fedha nyingi.
Anasema kuwa pale inapotokea kuwa mkulima wa Bangi aliyekodishwa hakufanikiwa kuvuna Bangi kutokana na Bangi hiyo kuharibika kutokana na ukame au kuharibiwa na vyombo vya dola, mkulima huyo hutakiwa kurudisha fedha alizopewa na wakala wake ambapo ili kupata fedha ya kurudisha, mkulima huiba ng’ombe za koo jirani na kuuza.
Waziri huyo anasema kutokana na mapigano hayo jumla ya watu 136 walifariki na zaidi ya 336 walijeruhiwa huku nyumba 2421 zikichomwa moto na kuacha zaidi ya kaya 756 zikiwa hazina mahali pa kuishi na vihenge 673 vya kuhifadhia mahindi kuchomwa moto katika kipindi cha kuanzia mwaka 2001 hadi machi mwaka huu.
Anazitaja hatua ambazo serikali imeshazichukua kuwa ni pamoja na kuifanya wilaya za Tarime na Rorya kuwa mkoa wa Kipolisi ili kukabiliana ipasavyo na matishio ya usalama, uhalifu na wahalifu.
Hatua nyingine ambayo Waziri Masha anaitaja kuwa ni ile ya serikali ya mkoa kupitia Tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI), kufanya kampeni mbalimbali kwa kushirikiana na taasisi nyingine zikiwemo za dini, wanasiasa, wizara ya elimu na kushawishi wananchi kuachana na mapigano. Waziri Masha anasema kuwa mikutano ya ujirani mwema baina ya Vyombo vya dola vya Tanzania na Kenya inaendelea kufanyika ili kuimarisha mahusiano miongoni mwao, ambapo mapema mwezi.
HAYA AKINA MURA KAZI KWENU BWANA, IRA MUBADIRIKE ETI!
Tuesday, April 21, 2009
JAMANI, Ndugu zangu mnaombwa kumsaidia huyu mpendwa Anaumwa!
MLEMAVU wa ngozi Mariamu Obedi (18)mkazi wa eneo la Nkhungu mjini Dodoma ameiomba Serikali pamoja na wanachi wamsaidie fedha kwaajili ya matibabu ya kansa ya jicho ili aweze kwenda hospitali ya Ocean Road ya jijini Dar-es-Salaam kutibiwa.
Ombi
Alikielezea kuanza kuugua jicho
Mariamu alisema kuwa baada yakuona hali hiyo ikizidi kuendelea aliamua kwenda katika hospitali kuu ya Mkoa wa
Mlemavu huyo wa ngozi (albino) alifafanua kuwa alianza kuumwa mwaka 2007 ambapo alipoenda katika hospitali hiyo ya mkoa wa
Alisema kuwa baada ya kwenda katika hospitali hiyo ya Mvumi pia walishindwa kumtibia na hivyo kumuandikia barua wakimtaka aende jijini Dar-es-Salaam katika hospitali ya Msasani ambapo alikwenda na kufanyiwa oparesheni na kupata nafuu.
Alibainisha kuwa baada ya kupata naafuu alirejea tena
Mariamu anafafanua kuwa alipofika katika hospitali hiyo alipimwa na hivyo kuonekana kuwa ana ugonjwa wa kansa ambapo anatakiwa kwenda hospitali ya Ocean road kutibiwa.










