Monday, November 09, 2009

Monday, September 21, 2009

MAPENZI hayana umri jamani, hebu msome mzee wa miaka 70 aliyejinyonga kwa wivu wa mapenzi!

Na Martha Mtangoo, Dodoma

9/21/2009

MZEE wa miaka 70 aliyefahamika kwa jina la Msuliche Mhogo amejinyonga kwa kutumia kamba kutokana na wivu wa mapenzi.

Kamnda wa polisi mkoani hapa Zelothe Steven aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 2.30 asubuhi katika kijiji cha Ngh’ambi wilayani Mpwapwa.

Akielezea tukio hilo Kamanda Zelothe alisema kuwa chanzo cha mzee huyo kujinyonga ni kutokana na wivu wa kimapenzi kwa mkewe mwenye umri wa miaka (30) ambaye jina lake limehifadhiwa.

Alifafanua kuwa kwa muda mrefu mzee huyo alikuwa akihisi mkewe ana uhusiano wa kimapenzi na mwanaume mwingine hapo kijijini ambaye ni jirani yake.

Alisema kuwa awali kabla ya tukio hilo kutokea , usiku mzee huyo aligombana na mkewe kuhusu mtoto wao mmoja ambaye ana umri wa miaka miwili akidai kuwa mtoto huyo ni wa mwanaume ambaye nahisi anatembea naye na si mwanaye.

Kamanda Zelothe alisema kuwa wakati wakiendelea na ugomvi huo mke mkubwa wa mzee huyo alienda kuamua ugomvi huo na ilipofika asubuhi mzee huyo aliaga kuwa anaenda safari na ndipo alipokwenda kwenye mbuyu ambao upo jirani na nyumbani kwake na kujinyonga.

Wakati huohuo jeshi la polisi mkoani hapa linamshikilia Hamis Salum (27) mkazi wa Manispaa ya Moshi kwa tuhuma za kufungua duka na kuiba simu 10 za aina mbalimbali.

Kamanda Zelothe alisema kuwa baada ya kufungua mlango mtuhumiwa huyo alijfungia ndani ya duka hilo na kuanza kukusanya simu dukani humo ambapo mwenye duka ambaye ni Freeman Narcis (23) alifika dukani hapo na alipofungua duka alimkuta mtuhumiwa huyo akiendelea kukusanya vitu katika duka hilo .

Kamanda Zelothe alisema kuwa jeshi hilo bado linamshikilia mtu huyo kwa mahojiano zaidi na atafikishwa mahakamni mara baada ya uchunguzi kukamilika.

Ends……

Thursday, August 20, 2009

Ningekuwa Spika Sitta Ningejiuzulu!


NINGEKUWA SPIKA SITTA NINGEJIUZULU

HAKI ya Mungu kweli duniani kuna mambo pamoja na mambo yote mazuri ambayo spika wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania Samuel Sitta kwa Wabunge wa chama cha mapinduzi wakiwemo na Mafisadi ambao wanajulikana kwa majina mimi sitaki kuwataja bado wabunge hao ambao wengine ni wajumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (NEC) na mafisadi wamo wamememgeuka!

Jamani kwa kweli ni lazima tukajifunza ustaarabu mengi sita kawasaidia wabunge hawa pamoja na wale wa upinzani lakini sasa tena moto umemgeukia yeye jamani kweli hii ni fair?
Hapa naorodhesha tu mambo machache ambayo spika sitta amewapigania wabunge hawa na kubalansi Bunge ili liliemee upande mmoja halafu akaonekana kana kwamba anapendelea upande mmoja wa CCM!

Spika huyuhuyu ambaye anaitwa Mbabe amepigania kwa nguvu marupurupu ya wabunge na kusababisha sasa hivi wabunge kulipwa mshahara tu kiasi cha sh. Milioni 12 kwa mwezi na marupurupu kibao!

Hiyo haikutosha spika huyohuyo mbabe amepigania mpaka sheria ya kuanzishwa mfuko wa maendeleo ya Jimbo kwa wabunge umepita kwa mbinde Bungeni licha ya wananchi kuonyesha kuukataa!

Mimi sijatumwa na Mtu kuzungumzia hili suala ila nimeguswa na kitendo alichofanyiwa hivi karibuni Mjini Dodoma katika Ukumbi wa Nec wa kutaka avuliwe uanachama kwa kuwa anaendesha eti Bunge kibabe!

Kwa kweli CCM hamkumfanyia Spika wenu sawa kabisa kwa sababu mnataka aliendesheje Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambalo hivi sasa limekuwa kama Kikundi cha vichekesho cha orijino Komedi kuna jambo lingine zaidi ya hili si mseme?

Alichokisema hivi karibuni Bungeni spika kuwa anaomba ulinzi wa ziada kwa kuwa nguvu ya mafisadi inamzidi alikuwa sahihi kwa kuwa tayati alishaona nini kinafuata na kwa kuwa serikali haikumuelewa ndiyo maana ilipuuzia na maneno meengi ya kejeli yakatolewa juu ya kauli yake!

Lakini ukweli wa maneno ya Mzee Sitta sasa yamejidhihirisha ndani ya mkutano wa CCM ambamo kunaonekana kuwa CCM bila mafisadi haiwezekani kuwa hai, sasa mnataka spika aendesheje Bunge lenu JAMANI?

Mnataka spika atoe uhai wake ndiyo mbaini kuwa alikuwa anaendesha bunge kwa usawa na kubalansi pia au mnatakaje au aendeshe Bunge kwa kupendelea wabunge wa CCM? Mtalishusha hadhi na viwango pia kama mnataka liwe ambavyo ninyi mnataka liwe!
Kwa hali hii mimi ningekuwa Spika Sitta ningejiuzulu Uspika ili kuwaachia nafasi mafisadi kumtafuta spika ambaye wao wanamtaka ambaye hatendesha Bunge kibabe au sio na kupendelea CCM maana viwango ulivyoahidi mwaka ule havitakuwepo tena!

Kwa kweli inauma halafu inakera zaidi inatia kichefuchefu kufanya hivyo ni kuonyesha ni kiasi gani kwamba CCM inashikiliwa na kuendeshwa na watu wachache wenye pesa zao na utartibu huu ambao CCM mmeuonyesha sijui nini kitafuata lakini mmetia DOA tena doa lenyewe jekundu kwenye nguo nyeupe!

SHAURI YENU CCM angalieni msije mkajuta kwa kuwasafisha watu ambao tayari walishachafuka siku nyingi kupitia watu ambao wangekusaidieni kuwasafisha angalau kwa kutumia busara zao ambazo zinaonekana ni ubabe!



Tuesday, June 23, 2009

Wasamalia wema wamsaidia Binti Mariam




Picha kushoto; Mwandishi na mmiliki wa Blog hii Martha Mtangoo, akimkabidhi fedha taslim sh. 230,00 Mariam ambaye alikuwa akihitaji msaada kwa ajili ya kufanyiwa operesheni ya saratani ya Jicho ambayo tayari ameshafanyiwa, fedha hizo
ambazo zimetolewa na wasamalia wema Hinai Tamim na Said ambao wanaishi nchini Oman.
Mungu awabariki sana.

Tuesday, May 05, 2009

WENZETU HUKO TARIME wanadumisha mila kwa mtindo huu

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI LAWRANCE MASHA
AMA kweli ukistaajabu ya Mussa uyaona ya Firauni! wakati watu wanapinga mila na desturi zilizopitwa na wakati huko TARIME wenzetu wanadumisha tu!
hebu soma hii kwanza.

Katika mkoa wa Mara kuna mila ambayo imekuwa ikifanywa na wazee wa kimila ambao kutokana na kutekeleza mila hizo matukio ya mauaji yamekuwa yakisababishwa na mapigano ya koo mbalimbali.
Mila hiyo imesababisha hali ya ulinzi na usalama mkoa ni mara kutokuwa shwari na kutoridhisha kutokana na matukio ya mara kwa mara ya mauaji ya kiukoo, wizi wa mifugo, ujambazi wa kutumia silaha na biashara ya madawa ya kuelevya hususan kilimo cha Bangi.
Wazee wa Kimila Mkoani Mara ndiyo viongozi na waamrishaji wa mapigano ya koo yanayondelea, ambapo wazee hao hunufaika na mapigano hayo kwa kupata mgao wa mali zilizoporwa katika mapigano.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrance Masha anasema kuwa mila na desturi za baadhi ya makabila zinachochechea mapigano baina ya vijana wa koo moja na koo nyingine vitendo ambavyo vimekuwa vikiheshimika miongoni mwa jamii hizo kuwa ni vya kishujaa.
Waziri Masha anasema kuwa wazee wa kimila wamekuwa viongozi na waamrishaji wa mapiganmo hayo ambapo wamekuwa na maradaka makubwa katika Koo zao na hutoa adhabu kali kwa vijana wanaokwepa kushiriki mapigano.
Waziri Masha anasema kuwa kutokana na hilo, hadi sasa hali ya ulinzi na usalama katika mkoa wa Mara si ya kuridhisha kwa kuwa kumekuwa na matukio ya mara kwa mara ya mauaji ya kiukoo, wizi wa mifugo, ujambazi wa kutumia silaha na biashara ya madawa ya kulevya hususan kilimo cha bangi.
Anasema kuwa matukio hayo yameenea katika wilaya za Tarime, Rorya na wilaya ya Musoma vijijini ambapo koo za hunyaga na Wamera na koo za Waanchari na Warenchoka na Wakira na Wanyabasi na Wairegi zimekuwa zikipigana mara kwa mara.
Masha anasema kuwa kilimo cha Bangi ambacho kimekuwa ni chanzo kikubwa cha uchumi kwa baadhi ya makabila katika mkoa wa Mara, pia kimekuwa ni chanzo cha mapigano hayo ambapo imekuwa ni kawaida kwa watu katika maeneo hayo kukodishwa na wakala kulima bangi na kulipwa fedha nyingi.
Anasema kuwa pale inapotokea kuwa mkulima wa Bangi aliyekodishwa hakufanikiwa kuvuna Bangi kutokana na Bangi hiyo kuharibika kutokana na ukame au kuharibiwa na vyombo vya dola, mkulima huyo hutakiwa kurudisha fedha alizopewa na wakala wake ambapo ili kupata fedha ya kurudisha, mkulima huiba ng’ombe za koo jirani na kuuza.
Waziri huyo anasema kutokana na mapigano hayo jumla ya watu 136 walifariki na zaidi ya 336 walijeruhiwa huku nyumba 2421 zikichomwa moto na kuacha zaidi ya kaya 756 zikiwa hazina mahali pa kuishi na vihenge 673 vya kuhifadhia mahindi kuchomwa moto katika kipindi cha kuanzia mwaka 2001 hadi machi mwaka huu.
Anazitaja hatua ambazo serikali imeshazichukua kuwa ni pamoja na kuifanya wilaya za Tarime na Rorya kuwa mkoa wa Kipolisi ili kukabiliana ipasavyo na matishio ya usalama, uhalifu na wahalifu.
Hatua nyingine ambayo Waziri Masha anaitaja kuwa ni ile ya serikali ya mkoa kupitia Tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI), kufanya kampeni mbalimbali kwa kushirikiana na taasisi nyingine zikiwemo za dini, wanasiasa, wizara ya elimu na kushawishi wananchi kuachana na mapigano. Waziri Masha anasema kuwa mikutano ya ujirani mwema baina ya Vyombo vya dola vya Tanzania na Kenya inaendelea kufanyika ili kuimarisha mahusiano miongoni mwao, ambapo mapema mwezi.

HAYA AKINA MURA KAZI KWENU BWANA, IRA MUBADIRIKE ETI!

Tuesday, April 21, 2009

JAMANI, Ndugu zangu mnaombwa kumsaidia huyu mpendwa Anaumwa!


MLEMAVU wa ngozi Mariamu Obedi (18)mkazi wa eneo la Nkhungu mjini Dodoma ameiomba Serikali pamoja na wanachi wamsaidie fedha kwaajili ya matibabu ya kansa ya jicho ili aweze kwenda hospitali ya Ocean Road ya jijini Dar-es-Salaam kutibiwa.

Ombi hilo alilitoa jana wakati alipokuwa akizungumza na mmiliki wa blog hii mjini Dodoma huku akilia kutokana na maumivu makali anayoyapata yanayosababishwa na uvimbe uliopo katika jicho lake la kushoto kuuma.

Alikielezea kuanza kuugua jicho hilo alisema kuwa kilitokea kiupele kidogo katika jicho hilo na hivyo kuanza kuvimba ikiwa ni pamoja na kumsababishia maumivu makali.

Mariamu alisema kuwa baada yakuona hali hiyo ikizidi kuendelea aliamua kwenda katika hospitali kuu ya Mkoa wa Dodoma kwaajili yakupata matibabu.

Mlemavu huyo wa ngozi (albino) alifafanua kuwa alianza kuumwa mwaka 2007 ambapo alipoenda katika hospitali hiyo ya mkoa wa Dodoma uongozi wa hospitali hiyo ulimwandikia barua aende hospitali ya Mvumi.

Alisema kuwa baada ya kwenda katika hospitali hiyo ya Mvumi pia walishindwa kumtibia na hivyo kumuandikia barua wakimtaka aende jijini Dar-es-Salaam katika hospitali ya Msasani ambapo alikwenda na kufanyiwa oparesheni na kupata nafuu.

Alibainisha kuwa baada ya kupata naafuu alirejea tena Dodoma anapoishi ambapo alikaa kwa muda wa mwaka mmoja ambapo ni 2008 na ilipofika mwaka huu hali hiyo ilimrudia tena na hivyo kulazimika kurudi tena katika hospitali kuu ya mkoa wa Dodoma.

Mariamu anafafanua kuwa alipofika katika hospitali hiyo alipimwa na hivyo kuonekana kuwa ana ugonjwa wa kansa ambapo anatakiwa kwenda hospitali ya Ocean road kutibiwa.

Hata hivyo ameiomba Serikali na watu wenye mapenzi mema ambao wataguswa na tatizo alinilonalo, kumsaidia chakula kutokana na mama yake mzazi Cahrerine Peter kutokuwa na uwezo hali ambayo inamsababisha kulala njaa licha ya yeye kunywa dawa kali na hivyo kumfanya kukosa nguvu kutokana na kukosa chakula.

KAMA UMEGUSWA KUMSAIDIA BINTI HUYU, TAFADHALI WASILIANA KUPITIA NAMBA HII' +255713358273, AU tumia akaunti hii 029201039794, NBC Bank Mazengo Branch.

Mungu akubariki sana.

Tuesday, December 02, 2008

Jamani ee wauza nyama Dodoma wametugomea tena wenzenu , tukitaka nyama mpaka twende Dar es Salaam!

JAMANI mlioko ughaibuni huku wenzenu karibu na waume zetu wanagoma ndani ya nyumba sijui itakuwaje, baada ya migogomo kufanyika katika maeneo mbalimbali hapa nchini zikiwemo sekta nyeti kabisa, hatimaye wafayabiashara wa Ng'ombe na uchinjaji wamegoma kuchinja ng'ombe kwa muda usiojulikana, kwa maana hiyo Dodoma hatuli nyama tena hadi watakapoamua sijui itakuwa lini hiyo, hebu Jimuvuzishe hapa kwa habari zaidi!

Na Martha Mtangoo, Dodoma

12/2/2008

UMOJA wa wafanyabiashara wa uchinjaji Ng’ombe Dodoma, (UWANDO), wamesitisha huduma ya kuchinja Ng’ombe na kuuza nyama kutokana na kupandishwa ushuru katika machinjio ya kisasa na hivyo kuufanya mji wa Dodoma kukosa nyama kwa muda usiojulikana.

Wafanyabiashara hao wamepandishiwa ushuru kutoka sh 10,000 waliyokuwa wakilipa awali hadi kufikia sh 20,000 kwa ng’ombe mmoja kuanzia juzi.

Wakiongea na waandishi wa habari jana katika eneo la mnada wa mifugo wafanyabiashara hao walisema kuwa walikuta tangazo juzi katika machinjio ya kisasa kuwa kuanzia juzi wanatakiwa kulipia huduma ya uchinjai y ash 20000 kwa kila Ng’ombe.

Mwenyekiti wa UWANDO Taita Ikoyi, alisema kuwa baada ya kuona tangazo hilo walishtushwa na kuamua kusitisha uchinjaji wa Ng’ombe kutokana na gharama za uchinjai kuwa kubwa ikilinganishwa na bei ya mifugo ilivyo sasa.

“Sisi hatujagoma ila tumeamua kusitisha huduma ya kuchinja mifugo yetu na kupeleka nyama katika mabucha kutokana na bei ya ushuru kuwa kubwa, tunabebeshwa mzigo mkubwa sana tunaiomba serikali itufikirie na sisi wadau itupunguzie ushuru” alisema Taita.

Naye Katibu wa UWANDO, Charles Laizer alisema kuwa tangu kujengwa kwa machinjio hiyo ya kisasa wamekuwa wakilazimishwa kupeleka mifugo yao kwenda kuchinjwa katika machinjio hiyo jambo ambalo limekuwa likiwakandamiza mno.

Laizer alisema kuwa awali baada ya kuanzishwa kwa machinjio hiyo walielezwa kuwa kuna uchinjai wa aina tatu ambapo moja ya uchinjai huo ulikuwepo ule wa kawaida kwa wafanyabiashara ambapo walitegemea uchinjaji huo ungekuwa wa bei y ash 1500 kama ilivyokuwa hapo awali lakini imekuwa tofauti na matarajio yao.

“Kama hali yenyewe ndio hii ni bora manispaa ijenge machinjio nyingine yenye ushuru wa bei nafuu na sisi wadu pia tuko tayari kujenga machinjio yetu ilimradi serikali itueleze utaratibu ukoje”alisema.

Naye Kaimu Meneja wa machinjio hiyo Florian Tillya alikiri kupandishwa kwa ushuru katika machinjio yake na kudai kuwa hali hiyo imetokana na mwekezaji ambaye anamiliki macnjio hiyo kampuni ya ya uwekezajiNICO kwa pamoja na Ranchi ya taifa ya NARCO.

Tillya alisema kuwa wafanyabiashara hao walipewa taarifa ya kupandishiwa bei ya ushuru tangu tarehe 8 Novemba mwaka huu machinjio hiyo ilipobinafsishwa na kuwa ushuru huo ulitakiwa kulipwa tangu kuanzishwa kwa machinjio hiyo mwaka 2003 lakini serikali ilikataa na ilikuwa ikitoa ruzuku y ash 9000 na fedha zilizoba walikuwa wakilipia wafanyabiashara hao.

Alisema kuwa kupanda kwa ushuru huo kunasababishwa na gharama za uendeshaji wa machinio kupanda ambapo alisema kuwa bei ya mafuta, na mishahara ya wafanyakazi viko juu kwa hiyo mwekezaji ameamua kupandisha ushuru kuanzia Desemba moja.

Ends………

Friday, July 04, 2008

Friday, June 13, 2008

BAJETI 2008/2009, SERIKALI imeshindwa kupunguza bei ya mafuta!


SERIKALI imeshindwa kupunguza bei ya petroli na dizeli katika bajeti yake ya mwaka 2008/2009, badala yake imewabana wavuta sigara na wanywaji wa bia na soda kwa kupandisha kodi ya bidhaa hizo.
Pamoja na kutoongeza ushuru katika bidhaa za petroli, bado wachambuzi wa masuala ya uchumi wanaona hali itaendelea kuwa ngumu katika sekta za uzalishaji na usafirishaji kutokana na kuongezeka kwa kasi bei ya nishati hiyo katika soko la dunia, hivyo wananchi kuendelea kuishi katika hali ngumu katika kipindi cha mwaka huu wa bajeti.
Bajeti hiyo pia imeongeza ushuru wa bidhaa katika huduma za simu za mkononi kutoka asilimia saba ya gharama ya matumizi ya huduma hadi asilimia 10. Kwa mantiki hiyo, gharama za matumizi ya simu zitaongezeka kwa watumiaji.
Akiwasilisha, mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2008/2009 bungeni jana, Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo hata hivyo, alitangaza kufutwa na kupunguzwa kwa kodi kadhaa zikiwemo za pembejeo za kilimo na ushuru wa magari, gesi na mafuta ya viwandani.
Kwa mujibu wa bajeti hiyo, vinywaji baridi vimeongezwa ushuru kutoka Sh48 kwa lita hadi Sh54, bia inayozalishwa Tanzania ambayo haijaoteshwa imepanda kutoka Sh173 kwa lita hadi Sh194, bia nyingine kutoka Sh 294 hadi Sh 329 na mvinyo uliotengenezwa kwa zabibu iliyozalishwa nje ya nchi kwa kiwango kinachozidi asilimia 25, kutoka Sh940 hadi Sh1,053.
Bidhaa nyingine zilizopanda bei ni vinywaji vikali kutoka Sh1,394 kwa lita hadi Sh1,561, sigara zisizo na kichungi na zinazotengenezwa kwa tumbaku inayozalishwa nchini kutoka Sh4,775 hadi Sh5,348 kwa sigara 1,000; sigara zenye kichungi na zinazotengenezwa kutokana na tumbaku inayozalishwa hapa nchini kutoka Sh11,266 hadi Sh12,618 kwa sigara 1000, sigara nyingine zimepanda kutoka Sh20,460 hadi Sh 22,915 kwa sigara 1,000 na tumbaku iliyo tayari kutengeneza sigara pia imepanda bei kutoka Sh10,333 hadi Sh11,573 kwa kilo.
Aidha, serikali imefanya marekebisho ya kodi ya kima cha chini cha mshahara na kutangaza kwamba kuanzia sasa mshahara usiozidi Sh100,000 hautatozwa kodi. Awali, kima cha chini kilichokuwa hakitozwi kodi kilikuwa Sh80,000.
Hata hivyo, wafanyakazi wanaopata mshahara wa zaidi ya Sh720,000 wameongezewa kodi na sasa watalipa Sh120,000 kuongeza asilimia 30 ya kiasi kinachozidi Sh720,000.
Akizungumzia bidhaa zilizofutiwa ushuru, Mkulo alisema kwamba serikali imesamehe ushuru wa forodha kwenye majembe ya mkono pamoja na pembejeo nyingine zote za kilimo zinazoagizwa kutoka nje ili kupunguza mzigo wa gharama kwa wakulima hasa wale wadogo.
Alisema uamuzi wa kusamehe kodi hiyo upo katika mapendekezo ya marekebisho ya viwango vya Ushuru wa Pamoja wa Forodha yaliyojadiliwa pamoja na na nchi za Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi katika kikao cha maandalizi ya Bajeti cha Mawaziri wa Fedha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kilichofanyika Juni 2, 2008 Jijini Nairobi.
Kodi nyingine iliyofutwa ni ya lami ambayo kwa mujibu wa Mkulo,
imelenga kupunguza gharama za ujenzi wa barabara, mafuta mazito yanayotumika kama nishati ya kupikia kama Moto Poa, gesi asilia iliyosindikwa na mitungi ya kuhifadhia gesi hiyo, kama ilivyo hivi sasa kwa gesi ya kupikia ya LPG, ili kuhamasisha matumizi ya gesi hiyo badala ya mafuta ambayo ni ghali, au mkaa ambao unaharibu mazingira.
Pia serikali imefuta Kodi ya Ongezeko la Thamani kwenye magunia yanayotengenezwa hapa nchini kwa ajili ya kuhifadhi nafaka na kutoa msamaha wa ushuru wa forodha kwa magari yaliyotengenezwa maalum kwa ajili ya ukusanyaji takataka yatakayonunuliwa na Serikali za Mitaa au mawakala walioidhinishwa na Serikali za Mitaa.
Mkulo alisema serikali imeondoa ushuru wa forodha wa asilimia 10 kwenye mafuta ghafi ya kula. Lakini mafuta yaliyosafishwa kidogo yataendelea kutozwa ushuru wa asilimia 10. Alisema hatua hiyo itaviweka viwanda vya mafuta nchini katika nafasi nzuri ya kiushindani na vile vya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Pia imepunguza ushuru wa mafuta mazito ya HFO, kutoka Sh117 kwa lita hadi Sh97 ili kupunguza gharama za uzalishaji viwandani na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko.
Kuhusu kodi za magari, Waziri huyo alisema kwamba serikali imepunguza ushuru wa magari kutoka asilimia 10 kwa magari yenye ukubwa wa injini unaozidi cc2000 na kuwa na viwango viwili vya asilimia tano na asilimia 10.
Katika mabadiliko hayo, magari yenye ujazo wa injini usiozidi cc1000 hayatalipiwa ushuru wa bidhaa huku yale yenye ujazo wa injini unoazidi cc1000, lakini hauzidi cc2000, yatalipa ushuru wa asilimia tano ya thamani ya gari, na magari yenye ujazo wa injini unaozidi cc2000 yatalipiwa ushuru wa asilimia 10.
Mkulo alisema katika mwaka huu wa fedha, serikali inatarajia kukusanya Sh7,216,130 bilioni na kutumia asilimia 64 ya bajeti yote kushughulikia miundombinu ya uchumi na huduma za jamii.
Matumizi ya serikali kwa mwaka 2008/09 yatakuwa Sh7,216.130 bilioni ambayo ni jumla ya matumizi ya kawaida ya Sh4,726.650 bilioni na matumizi ya maendeleo ya Sh2,489,480 bilioni.
Alisema serikali pia imetenga fedha kwenye maeneo muhimu kwa kuzingatia vipaumbele na mipango ya kitaifa ambayo ni Elimu iliyotengewa Sh1.43 trilioni, Miundombinu ya barabara Sh973.3 bilioni, afya Sh 803.8, Kilimo Sh460.0 bilioni, maji Sh 230.6 bilioni na Nishati Sh383.4 bilioni.
Mbali na maeneo hayo pia kuna fedha zitakazotumika kutekeleza Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUKUTA) katika nyanja za utawala bora, ulinzi na usalama, malipo ya madeni, pensheni na Bima ya Afya.
Waziri Mkulo alitaja kupanda kwa bei ya mafuta ya petroli, nafaka, pembejeo za kilimo na malighafi za viwandani kuwa changamoto zitakazoikabili bajeti ya mwaka huu ingawa serikali imejipanga vizuri kukabiliana na changamoto hizi.
Alisema ongezeko la bei ya bidhaa hizo limesababisha kasi ya mfumuko wa bei karibu katika kila sekta na kuvuruga masoko ya fedha ya kimataifa jambo ambalo limeathiri mtiririko wa vitega uchumi (FDI) kutoka nchi tajiri kuja nchi maskini
Changamoto nyingine ni kuongeza mapato ya ndani na kudhibiti kukua kwa haraka kwa bajeti ya kawaida, ili kuanza kujitegemea.
Alisema utegemezi wa bajeti kwa wahisani ni tatizo kwani michango na misaada yao haifiki kwa wakati hivyo kuna haja serikali kupunguza kasi ya kuongezeka kwa matumizi ya kawaida, hasa yale yasiyoweza kurekebishwa iwapo mapato yatapungua.
''Kwa hiyo, kunahitajika umakini mkubwa katika kuhimili athari za hali hii ya uchumi wa dunia. Hata hivyo, nchi zinazozalisha mafuta ya petroli zinategemewa kuendelea kunufaika na ongezeko la bei ya mafuta hasa kwa kuwa mahitaji ya nchi kama China, India na Brazil ni makubwa,'' alisema.
Hata hivyo, alisema serikali imeandaa mikakati kadhaa ya kukabiliana na hali hiyo ikiwamo kupunguza utegemezi kutoka asilimia 42 mwaka jana hadi asilimia 34 mwaka huu.
Alisema pia serikali itahakikisha upatikanaji wa nafaka ambazo bei zake zinapanda kwa kasi na kuathiri maisha ya wananchi na kusitisha usafirishaji nje wa bidhaa hizo, ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya usafiri vijijini, ili kupunguza gharama za kusafirisha chakula hadi kwenye maeneo ya soko.
Alishauri kutumia ongezeko la bei ya chakula duniani kama fursa ya kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula nchini, kwa kuhimiza kuwekeza katika mashamba makubwa na kuhimiza wananchi walime chakula kwa wingi ili kujipatia chakula na kipato.
Lete maoni yako kuhusiana na Bajeti ya Serikali kwa mwaka mpya wa fedha 2008/2009 karibu saaaana!

Wednesday, April 02, 2008

JAMANI Sikujua kama ndugu zangu Wagogo tuna uchungu na mifugo namna hii!!! hebu soma hii halafu unipe jibu!!1

MFUGAJI mmoja amekufa baada ya kunywa sumu aina ya Daimeko baada ya kukuta mkewe na mfanyakazi wake wakiwapiga ng’ombe wake.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa Michael Kamhanda aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa Mfugaji huyo Philemoni Mkunaa (35), alikunywa sumu hiyo baada ya kuona kuwa ng’ombe wake wanateswa.

Akielezea tukio hilo Kamhanda alisema kuwa siku ya tukio majira ya saa tisa usiku aktika kijiji cha Lamiti tarafa ya Mundemu wilayani Bahi, akitoka katika pombe Mkunaa alimkuta mkewe na mchungaji wake wa ng’ombe wakiwapiga ng’ombe hao ambapo aliwauliza kwa nini wanawapiga ng’ombe na kujibiwa kuwa wanawapiga ili waingie zizini.

Alisema kuwa baada ya kupewa jibu hilo mfugaji huyo alisema kuwa hawaoni kama wanavyowapiga ng’ombe hao wanawatesa na kama wanawatesa ng’ombe hao yeye atakuwa sumu ili afe.

Kamhanda alisema kuwa baada ya kuona bado ng’ombe wake wanapigwa Mkunaa aliingia ndani na kuchukua dawa aina ya Daimeko na kunywa na baada ya muda alianguka na kufariki.

Katika tukio lingine Jeshi la polisi linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kumpiga fimbo na kumuua mtu mmoja aliyejulika kwa jina la Yohana Chiloleti (16), mkazi wa kitongoji cha Makeweni wilayani Kongwa.

Kaimu kamanda Kamhanda alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira saa moja jioni baada ya Chiloleti kuchungia ng’ombe karibu na nyuma ya watuhumiwa hao.

Kamhanda alisema kuwa baada ya watuhumiwa hao kuona chiloleti akichungia ng’ombe karibu na nyumbani kwao walimhoji nkwa nini anachungia hapo na ndipo alipowajibu kuwa kwani kuna tatizo gani ndipo watuhumiwa hao walianza kumshambulia kwa kumpiga na fimbo kichwani hadi kufa.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Sisemi Mgoya (15), na Semarungo Mgoya (17), ambapo wanatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.

Ends………..

Sunday, March 30, 2008

Heri ya mwaka 2008

Nakuombeni saaana wapenzi wasomaji wangu jamani kwa kuwa kimya muda mrefu sasa, kwanza heri ya mwaka mpya! mimi niko safi sana majukumu tu ya kujiandaa kuwa mama ndiyo yananikaba lakini msijali nimerudi tena tegemeeni mambo mapya na mazuri na sasa yatakuwa ya kigogo zaidi si mnajua tena mtu kwao bwana wee na mkaa kwao mtumwa! nawashukuru sana wasomaji wangu ambao mmekuwa mkiwasliana na mimi na kutoa maoni na michango mbalimbali kwa ajili ya kuboresha web page hii, nakushukuru sana kakaangu George Kusila na wengine wote, karibuni mlango uko wazi napokea maoni yenu.

Thursday, October 18, 2007

ALBADIR dhidi ya UbaBE BuNgeNI!!

Baada ya ubabe ndani ya Bunge na kumuondoa Bwana Zitto Bungeni na Bunge kuvunjwa wale wote walio msakama na kumfanyia nyodo wamesha kutwa na haya yafuatayo;

Kwanza alianza Ruth Msafiri wa Muleba Kaskazini. Mumewe alipata ajali mbaya ya pikipiki na kukimbizwa Muhimbili na alifia hapo Mhuhimbili lakini haikutangazwa .

Baadaye Peter Selukamba akiwa anaendesha mwenyewe alinusurika kifo baada ya gari lake kuwa kama chapati yaani ile VX yake ya Ubunge na hadi sasa gari halitamaniki lakini akapona kuumia . Hawakuandika kokote wakafanya siri.

Siku hiyo hiyo Mbunge Malima akiwa anaendesha yeye mwenyewe akapata ajali pale uwanja wa JK Nyerere akanusurika kuumia lakini gari inahitaji matengenezo makubwa waandishi wa majira kimya hawajasema lolote . Baadaye akaja Mudhihiri wote mnayajua ya kwake.
Juzi kapata ajali mbaya sana ndugu Kumchaya Selemani wa Lulindi.Watu 2 wamekufa na yeye kanusurika .

We all have also heard about Juma Kapuya ……

Je hiki ni kitu gani ? Mungu kutupigania Watanzania ?

Je kwa nini vyombo vya habari visiandike? Au Albadir ilyosomwa na watu wa mwisho wa reli si mchezo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Jamani waheshimiwa kuweni makini wakati wa kuongea maisha haya huwa mafupi pale yanapoanza kuwa matamu!

Saturday, August 18, 2007

KUMUMUVUZISHA ZITTO KABWE KUMEMPANDISHA CHATI, SASA YUKO JUU


KUMUMUVUZISHA Zitto Kabwe, Kumempandisha Chati, sasa yuko Juu!!!!!



Kama Wabunge waliounga mkono Mh. Zitto Kabwe asimamishwe walifikiri wanamkomoa, basi hali ni tofauti kwani wananchi kibao wamemuunga mkono.


Baadhi ya Wabunge wakichangia mjadala wa kumsimamisha walisema anatumia Bunge kujipatia umaarufu wa kisiasa kumbe wenyewe ndio wanampatia umaarufu kwa kumtimua.Wananchi wengi wamechukizwa na kitendo cha kumsimamisha Kabwe kwani wanahisi ni janja ya kuwafunga midomo baadhi ya Wabunge wenye nia ya kweli ya kufichua maovu.


Kuanzia wasomi wa Chuo Kikuu (Profesa Mwesiga Baregu, mhadhiri mwandamizi wa masuala ya siasa na ushirikiano wa kimataifa wa UDSM) wamesikitishwa na uamuzi huo wa Bunge.Prof. Baregu alisema kwa kitendo hicho, Bunge halikumtendea haki Kabwe, halikutenda haki kwa demokrasia na pia halikutenda haki kwa wananchi.


Alisema kumwadhibu mbunge huyo hakujaweza kuondoa ukweli kwamba kuna mikataba mibovu inayoingiwa na serikali na suala la Buzwagi ni mfano tu kati ya mikataba mingi mibovu iliyoingiwa, hasa ya madini.


Mwenyekiti wa Chama cha DP Mchungaji Christopher Mtikila pia ameungana na wenzake akisema Zitto hana kosa, adhabu aliyopewa ni uharamia wa demokrasia na suala ambalo kila Mtanzania anatakiwa kulitambua na kutotakubali kukaa kimya.


Naye Wakili wa Kujitegemea, Tundu Lissu, alisema adhabu iliyotolewa kwa Kabwe sio halali, huku akitaka mbunge huyo aruhusiwe kuendelea na vikao vyote vya Bunge.Akiongea kwa niaba ya Asasi za kiraia Lissu alisema ni bora Bunge likaeleza mbunge huyo amepewa adhabu ya ngapi ili wananchi walinganishe na kufahamu adhabu ambayo ilikuwa inastahili kulingana na kosa, kama analo.


Wengine waliohojiwa wamesema uamuzi huo ni sawa na kuwanyima haki wapiga kura wa Kigoma Kaskazini kwani watakosa mwakilishi kwa kipindi alichosimamishwa.Hivi sasa Mbunge huyo anawasiliana na baadhi ya wanasheria kuona uwezekano wa kukata rufaa Mahakama ya Rufaa kupinga adhabu hiyo.


Na katika kumwuunga mkono CHADEMA wanaandaa mapokezi ya Mbunge wao huyo pindi atakaporejea Dar akitokea Dodoma alikomuvuzishwa nje ya Bunge hadi Januari mwakani.


Huko Dodoma nako Wabunge wa upinzani wamekaa kikao cha dharura kutafakari cha kufanya baada ya mwenzao Kabwe kusimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge.Na katika kumuunga mkono Wabunge hao wa upinzani wamesema kuwa kila mwezi watakuwa wanamchangia karibu sh. milioni 1.5/- ili afanikishe kazi zake anazofanya za Ubunge.Katika adhabu aliyopewa Mbunge huyo atakuwa analipwa nusu mshahara hadi atakaporejea tena Bungeni kuendelea na vikao.

Friday, February 02, 2007

MLIOKO UGHAIBUNI WENZENU HUKU HALI NDIO IKO HIVI!!!!

JAMANI HUKU WENZENU HATUSAFIRI TENA!

Huu ni Msafara wa Naibu Waziri wa Miundombinu Dk. Milton Mahanga ambao ulikwama katika eneo la Isuna Mkoani Singida wakati akikagua barabara ya Dodoma-Manyoni, Manyoni-Singida, huku hali ni mbaya sana jamani wasomaji wangu na hasa nyie mlioko Ughaibuni akina Macha Ndesanjo. zaidi ya shilingi bilioni 45 zinahitajika kukarabati barabara hizi ili kurudi katika hali yake ya kawaida.

Monday, October 09, 2006

Tuesday, August 01, 2006

Kama Mnabisha muulizeni Michuzi!!!!

WELCOME!!!!!
Nikikwwambieni Wasomaji wangu niko Bize naomba muamini na kama hamuamini mumuulize Michuzi, ilibidi tu tuipige ili kuthibitisha kauli yangu niiyoitia kijiweni, hapa ni katika viwanja vya Bunge, Blogaz. (Michuzi kushoto na Martha D. M).

Monday, June 12, 2006

HAPA NI MHESHIMIWA MBUNGE NDO KAVAA HIVI JE ALIPOKUWA PAPARAZI KAMA MIMI ILIKUWAJE?????!!!!!!!!


MHISHIMIWA AMINA CHIFUPA MPAKANJIA(CCM)!!!!!!!
HAKI YA NANI, INASEMEKANA MBUNGE HUYU NDIYE ANAYEONGOZA KWA KUJIRUSHA KULIKO WABUNGE WENGINE AKIFUATIWA NA BIBIE HALIMA MDEE MBUNGE WA VITI MAALUM (CHADEMA). MBUNGE MWANAUME ANAYEPENDA KUJIRUSHA NA MWENYE UMRI MDOGO KULIKO WENGINE BADO SIJAMPATA KAMA KUNA MTU ANAFUNUNU HIZO BASI ANITONYE!

Tuesday, May 02, 2006

Uhuru wa Vyombo vya habari Tanzania Bado ni Ndoto.

Kila mwaka Mei 03 Wanaharakati kote ulimwenguni husherehekea Siku ya uhuru wa Vyombo ya habari Duniani Swali ni Je uhuru huu hapa Tanzania upo au bado longolongo? jadili bila jazba wala upendeleo karibu!!!!!!!!!!!

hivi ndivyo mzee wa sumo na mwenzie walivyoumizwa na askari magereza walipoenda kukava raia wanavyoondolewa kwa nguvu kwenye nyumba zilizokuwa za atc na kununuliwa na magereza kule ukonga. kesi iko inanguruma mahakamani kwani askari jela waliohusika walishtakiwa. Picha na Issa (Michuzi)

Monday, April 03, 2006

Amini! Gari ya hakimu iliyoibwa yapatikana!

Gari ya hakimu iliyoibiwaimepatikana eneo la Yombo Buza wilayani Temeke. Gari hilo limepatikana likiwa limeng'olewa Vipuri mbalimbali ikiwemo vyenye thamani ya sh. milioni 1.1.

Hakimu safari alisema kutokana na gari hilo kutokuwa na mafuta ya kutosha ndio sababu iliyowafanya wezi hao kuliacha gari hilo baada ya kuishiwa mafuta. Gari hilo linashikiliwa katika kituo cha polisi Chang'ombe na Polisi bado wanaendelea kuwasaka walioiba gari hilo!!!!!!!!! haya mnasemaje?????

Wednesday, March 29, 2006

HAKI ya nani, yaani kweli wabongo sasa tumedata, hebu soma hii kwa makini halafu ufikirie itakuwaje! HAKIMU Mkazi wa Kisutu Jijini Dar Es Salaam juzi Mahakamani aliibiwa gari lake aina ya Suzuki Samurai wakaiti akiendesha Kesi.

Gari hiyo lina thamani ya sh. Milioni 3.5 na aliibiwa akiwa Bize na Masuala ya Kesi Mahakamani hapo.

Hakimu Safari aliibiwa gari hiyo yenye namba za usajili T867 ALA, ambali inadaiwa liliibiwa saa nne asubuhi baada ya hakimu huyo kufika katika eneo lake la kazi na kuegesha.

Baada ya kumaliza shughuli zake za kikazi mahakamani hapo hakimu huyo alitoka nje ya jengo la mahakama akiwa na funguo za gari hilo kwa nia ya kurejea nyumbani na ndipo alipogundua kuibiwa kwa gari hilo.

hakimu huyo alisema kazi kulitafuta gari lake limo mikononi mwa polisi baada ya kuropoti kwa mkuu wa makosa ya jinai (RCO), gODFREY nZOWA ambapo alipatiwa RB namba CD/RB/3147/06.

HII NI KALI KULIKO YA MWANDOSYA AMBAYE ALIVAMIWA KIWA BAA HIVI ALIYEIBA GARI HIYO AKIKAMATWA NA KUFIKISHWA MAHAKAMNI HAPO KWA HAKIMU HUYO ALIYEIBIWA GARI YAKE ANAWEZA AKAPEWA ADHABU GANI???!!!!! INATISHA.