Saturday, August 20, 2005

Nikusikie tena unatishia watu Amani!


Inasemekana Vyama vya upinzani vinafanya fujo makusudi kutokana na wagombea wa Vyama hivyo kujua kuwa havitashinda katika uchaguzi Mkuu ujao.

Lakini kwa mujibu wa Wachunguzi wa masuala ya Siasa wanasema kuwa ni katika kujitetea tu ndio maana vyama hivyo vinafanya hivyo,

Je wewe Msomaji wa Blog hii una maoni gani? unafikiri ni kwa nini inakuwa hivyo? weka maoni yaklo hapa ili unisaidie kuelewa ni kitu gani kifanyika na kwa malengo hani hasa, unakaribishwa kuweka hoja zako bila jaza wala upendeleo wa aina yoyote.

Karibuni.

Tuesday, August 16, 2005

Ni kama anasema "Ndejembi Mwenzio najisikia Kizunguzungu nisaidie ninyanyuke hapa nisije nikaanguka!" Huyu Makamu Mwenyekiti wa CCM na Muasisi wa CCM Mzee Rashid Mfaume Kawawa ambaye jana alishindwa kuendelea kuhudhuria Mkutano Mkuu wa CCM almaarufu NEC kutokana na kuugua ghafla akiwa ukumbini. Mzee tunalkubali mchango wako saaana lakini pumzika sasa umechoka he! unataka kufa kishujaa?
Kwa habari zaidi Soma hapa.

Wednesday, August 03, 2005

HAYA TENA MABLOGST WANAZIDI KUONGEZEKA!!!!!

Ni waandishi wa Habari tu tena toka Dodoma, huyu nae ni Mpiga Picha wa ITV Dodoma naitwa Twaha kivale, Bonyeza hapa umsome.

Tuesday, August 02, 2005

Si Ulitaka Chai! Iweje ulalamike Unaungua?



Baada

Haya Jamani tukiambiwa tuache kunywa Chai kavu tunang'ang'ania Tu na Matokeo yake ndo haya Tunaungua, Kunywa chai na Vitafunio hata ikiwa ya Moto Kiasi gani huwezi Kuungua kama ilivyomuunguza marehemu Mrembo Huyo ambaye alikuwa akisoma Chuo Kikuu cha MOI huko Nchini Kenya.

Alipojijua kama ameambukizwa Virusi ya Ukimwi akaahidi Kulipiza Kisasi kwa yeyote ambaye atakatiza Machoni Mwake na alifanikiwa kuambukiza Jumla ya Wanaume 124 nchini humo ambao waliopona ni 6 kwa kuwa walimua kunywa chai na Vitafunio.

Kabla alikuwa Mrembo sana kama anvyoonekana katika Picha ya Chini
Nawaombeni sana Radhi Wapenzi wasomaji wa Blog yangu, kwa kuchapisha Picha ya Kutisha namna hii hii inasababishwa na Mimi kuguswa sana na Tukio hili.
Kunyweni Chai na Vitafunio Jamani la Sivyo Tutaungua!

Wednesday, July 27, 2005

KHA! Akina dada Tumelaaniwa au?


NAJUA, kuwa kila mtu anayetyembelea Web Page yangu anafahamu kuwa ni nini naongelea zaidi katika kila kurasa.

Sasa hili nililokutana nalo linaniytia uchungu sana, inaniuma sana ninapoona akina dada wenzangu wanafanya mambo ya ajabu wakati wamejaaliwa kila kitu yaani wamekamilika kila Idara.

Hebu angali sasa ni nini hiki? inaiuma sana kuona akina dada hatujithamini kabisa miili yetu, eti siku wanasema wapewa bure na lazima wapewe bure wewe usijidanganye kwa hilo na ulaaniwe.

Huyu ukimuuliza ni nini anafanya hapo atakwambia yuko kazini lakini hiyo kazi yako ya kucheza shoo ukivaa vizuri mbona itanoga tuuu? kilichomsibu sasa Soma hapa chini.


Mr Nice nusura amtwange mnenguaji wake!

MWANAMUZIKI mahiri katika miongoko ya Takeu ya kizazi kipya Lukas Mpenda almaarufu Mr Nice Ijumaa iliopita alimkwida mnengaji wake aliyetambulika kwa jina la Mpasi Mussa nma almanusura angemtwanga makonde.

Tukio hilo lilitokea kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa bendi ya Msondo Ngoma Music ambayo zamani ilikuwa ikiitwa OTTU Jazz. Mr Nice alimkunja mnenguaji wake akionekana kapndwa na hasira kitendo kilichofanyika nyuma ya jukwaa la ukumbi huo uliokuwa umehudhuria na mashabiki wengi.

Mr Nice alizua tafrani hiyo kwa madai kwamba mnenguaji wake huyo alikosa nidhamu kwa kudai pesa yake kwa utaratibu aliodai haukuwa wa heshima. "Inabidi nikuonye kutokana na utovu wa nidhamu ulioufanya, nakuonya kama mdogo wangu," alisikika akifoka Mr Nice.

Hata hivyo menguaji huyo aliomba msamaha na ndipo Mr Nice alipomwachia huku akisikika akimwambia: " Mimi sipendi kufanya kazi na watu kama nyinyi, sitaki kuwa pamoja na wewe kwa sababu umenidhalilisha."

Acha kazi kwani lazima ucheze Shoo? anza hata kuuza Vitumbua au Maandazi ukiwa na Msimamo maisha yatakunyookea mwenyewe utashangaa huwezi kuamni.

Haya kila la Kheri

Monday, July 18, 2005

Wizara Nyeti ambayo Waheshimiwa Wabunge hawaifahamu!!!


WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII

WIZARA ya Maliasili na Utalii ni Wizara NYETI ambayo watu wengine bado hawajatambua Unyeti wa Wizara hii, inaniuma sana.

Nafikiri kila mtu anajua ni kwa nini hilo linaniuma saaana, Utamaduni wetu watanzania ni pamoja na mali ya asili ambayo ni Misitu na hifadhi za wanyamapori.

Naumia sana kwa maana Utalii ni pamoja na Wanyamapori, Milima, Maziwa na Mito ambayo ipo hapa Tanzania.

Sasa hebu fikiria kinachonisikitisha zaidi ya yote ni kwamba hata Waheshimiwa Wabunge wenyewe wa Bunge la Jmhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (TANZANIA), hawajui kabisa kuwa Wizara hii ni Nyeti.

Utajuaje kama hawajui kuwa Wizara Nyeti sio Nyeti, ni hivi kwanza Wizara hii haina msaidizi kabisa, Mwanamama
ZAKIA HAMDANI MEGHJI anafanya kazi Mwenyewe kama Waziri wa Malisili na Utalii.

Ni kwamba wabunge walishindwa kushinikiza kuwa Wizara hiyo Nyeti iwe na Msaidizi yaani hapa naamnisha kuwa Wizara hiyo haina naibu waziri.

Mama huyu pamoja na kutokuwa na Naibu Waziri kama ilivyo wizara nyingi tu ambazo zingine zina manaibu Waziri watatu kama ilivyo Wizara ya Fedha anafanya vizur sana.

Angalia Watalii wameongezeka kutoka 295,312 mwaka 1995 hadi kufikia 582,807 mwaka 2004, hii ikiwa ni wastani wa ongezeko la asilimia 10 kwa mwaka.

Hali kadhalika mapato yatokanayo na utalii yameongezeka toka dola za kimarekani milioni 259.4 mwaka 1995 hadi Dola milioni 746.0 mwaka 2004 mabpo mpaka mwaka huo Sekta hiyo ilikuwa imetoa ajira kwa watu wapatao 199,000.

Sasa kwa nini mama huyu ambaye anautangaza utamaduni wa Mtanzania nje ya Tanzania asiwe na Msaidizi? Haya nikisema utasikia ooh wanawake bwana wanataka dezo hatutaki dezo na kazi tuweza sana, Hongera sana Mama Meghji kwa kazi nzuri.

Lakini ni vyema Serikali ya awamu ya nne ikazingatia ushauri huu kuipatia Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii kwa kuwa hii ni Wizara Nyeti kama zilivyo wizara nyingine ikiwezakana atoke Wizara ya Fedha azibe nafasi hiyo.

Angalia utalii wa Tanzania hapa uvayotangazwa bila upendeleo hiyo ikiwa ni kazi ya Mwanamama na mwaka huu anagombea hataki viti maalum tena!!!!!!!

Monday, July 11, 2005

Inapofikia hatua Mtoto Anazaa Mtoto Mwenzie!! What has become of mankind?

Ama kweli sasa tulipofikia ni Karibu na Mwisho, Hivi Yesu atarudi lini? kila mtua ana majibu yake wengine wanasema alisharudi wengine wanasema arudi kufanya nini yote Kheri lakini na tumuombe sana atausaidie kuelewa.

Hii ni picha ya Mtoto mwenye umri wa miaka 10 tu! wa Wilaya ya Kericho Nchini Kenya, kila mtu atauliza sasa kma wa Kericho Nchini Kenya si tufanyaje, Sikiliza ni Mtoto wa miaka 10m ambaye miezi michache iliyopita alikuwa akicheza na wenzie michezo mbalimbali akirudi Nyumbani anaogeshwa lakini sasa amekuwa mama wa Mtoto Jamani tunaenda wapi?!

Kinachoniuma zaidi ni kwamba Baba Mtu mzima ana akili zake ameamua kumfanyia hivi huyu mtoto mdogo ambaye ni sawa na mwanaye wa kumzaa jamani inatia uchungu sana sijui ni wapi tunaelekea Mungu tusaidie kuelewa nini Tunatenda.

Inauma sana, inakatisha tamaa, hebu fikiria mtoto mdogo namna hii anamnyonyesha mtoto mwenzie amezaa anaweza kulea? anaweza kujua iwapo leo mwanangu anaumwa sasa nimpeleke Hospitali? wewe Baba Jitu Zima umemtafutia matatizo ambayo yanamfanya mtoto anaingia katika kitabu cha historia wewe umepumzika.

Ukimuuliza alikuwa anatafuta nini kwa mtoto mdogo tena bado ananuka Shombo kali madai yake mtoto mdogo hana Ukimwi, hatakuwa na ukimwi wakati mizee mizima inataka watoto wadogo?

Na Walaaniwe wote wenye tabia mbaya inayomsababishia mtoto mdogo matatizo katika Siku zote za Maisha yake.
Unakaribishwa kuchangia Bila Jabza wala Upendeleao wa Kijinsia Karibu.

What has become of mankind?

This is a picture of a 10 year old lovely school girl,from the Kericho District in Kenya.
What makes her sospecial? With her whole life ahead of her, a wonderful futureto strive for an education and to move into her teenyears and have fun playing with her fellow girls,children of her own age, she is not playing withdolls.
She is handling the real thing. She has becomea Mother.
Definitely there is a Man somewhere who is to blame!What has become of mankind?People have no fear of the Creator, the Most Merciful,the most Benevolent.
Are we coming to the end?

Tuesday, July 05, 2005

Kwa Nini Sisi Tuweze tuna Nini na Nyie mshindwe mna nini? Mnannisikitisha sana, nyingine mpya hii hapa!!!!!!


NASIKITIKA sana kuona eti asilimia 95 ya Mablogist wa Kiswahili ni Waandishi wa Habari kwa nini lakini?

Mbona mnaifanya mioyo yenu kuwa migumu jamani, Kublog kiwahili sio dhambi, na kama siyo dhami haiwezi kuleta mauti zaidi ya kukupatia faida jamani kwa nini?

kama mnadhani mimi muonugo Fungua Blog nyingine hii hapa www.ngurumo.blogspot.com uone nini kunaendelea.

huyu anaitwa Ansbert Ngurumo ni Mwandishi wa habari Mwandamizi na Nzuri zaidi ni Mhariri wa Gazeti la Tanzania Daima Jumapili, kwa nini basi Madaktari, Maprofesa au hata Wakulima ambao vijiji vyenu vinaendelea mshindwe kuanzisha Blog zenu jama?

wala haihitaji fedha kwa ajili kuanzisha na kumiliki Blog, nawaombeni jamani Bogo si kwa ajili ya Waandishi wa habari ni kwa yeyote Mwenye nia ya kumiliki. msiogope jamani tafadhali msiogope.

Sunday, July 03, 2005

Junior naye Eti anasikiliza Nyeti ya Wagosi


WATOTO ni rika moja ambalo asipolelewa vyema basi ama atafanya maajabu ama madudu katika ulimwengu huu.

lakini pia utandawazi unaharibu sana watoto katika ulimwengu huu ambao wataalam wanauita ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia.

Sasa Hebu angalia Junior anasilikiza Music naelewa kweli halafu mziki wenyewe wa Wagosi wa Kaya, unaitwa 'NYETI'.

HIVI KWELI TUTAFIKA JAMANI?

Tuesday, June 28, 2005

Monday, June 20, 2005

Mila Hii itawamaliza Wamasai 'Katatumaliza Jamani'

WAMASAI ni kabila moja kubwa sana, na ni kabila moja ambalo limekuwa likijitahidi kuenzi na kudumisgha mila na Destutri ya kabila hilo hapa nchini.

Licha ya kufanya hivyo wa mila zao wamekuwa wakidumisha kwa staili ya ajabu hebu kaa mkao wa kula ushangae ya Musa.

MILA hii katika kabila la kimasai inawalenga vijana ambao wamekwishaoa ambao rika lao linaitwa MORANI.

MILA hii iko hivi yaani MORANI wa kimasai anapojisikia kufanya Ngono anakwenda katika nyumba yoyote ambayo ni kijana mwenzee mwenye mke.

Kabla hajaingia ndani ya Nyumba hiyo anachomeka Mkuki wake mlangoni halafu akiingia ndani anamkuta mama mwenye nyumba wanaanza kufanya Mapenzi.

Kila mtu anajua kuwa umasaini hakuna mipira ya Kiume yaani (condoms) wanashughulika bila kutumia zana ya aina yoyote hapa.

wakati wakiwa ndani wanafanya mambo hayo Baba Mwenye Nyumba akija anakuta Mkuki uko nje ya Nyumba yake anachofanya ni kuondoka zake na kuwaacha Adam na Eva wanafaidi Tundi.

Unajua akitoka hapo anakwenda wapi? akitoka hapa na yeye anakwenda katika Nyumba nyingine ambayo ana uhakika akienda atafanya kile ambacho mkewe anafanyiwa anafika anachomeka Mkuki nje anaanza kuvunja amri ya sita bila zana!!!!!!!!!!1

Sasa fikiria ni wamasai wangapi wapo Jijini Dar Es Salaam wanafanya kazi ya Ulinzi na wafanya Ngono na machangudoa wa kule Kinondoni kwa pesa ambazo wanapata.

Wakirudi umasaini wanagawa Virusi bila kujua kuwa wanavimiiliki ndani ya miili yao kwa wake wa wenzao ambao nao watavipata bila kujua kwa wake wa wenzao.

Kamchezo kazuri sana lakini kamejaa rafu za ajabu, yani hakuna refa wala mshika kibendera na mbaya zaidi hakuna hata wale wahudumu toka msalaba Mwekundu (RED CROSS), yaani ukichezewa rafu hakuna cha huduma ya kwanza wala nini!

Sasa kama tukidumisha Mila zetu kwa staili hii ni nani atabakia katika Tanzania hii ambayo uchumi umekua kwa asilimia 4?

Wakati umefika sasa tubadilike kuendana na Karne ambayo sasa ni Sayansi na Teknolojia na hatuko kabisa katika Zama za Mawe za Kale ati ee.

NGO's, CBO's na Serikali hebu iangalie suala hili kwa ukaribu zaizi katatumaliza haka ka UKIMWI jamani kwa kudumisha mila kwa sataili hii.

Sina hakika kama TACAIDS wana habari hii hebu walifuatilie basi hili jamani.

TAKE CARE!

Friday, June 03, 2005

Kwa nini wasanii hawa washike mbele tu kunani? mnamfundisha Junior tabia Mbaya..

OO! mziki wa kizazi kipya unakua! unakua kwa vigezo gani? hebu anganlia mambo yanayofanywa na wasanii hao halafu uchangie unakua kwa vigezo gani na kiwango kipi!

kwa nini iwe mbele tu? na siyo Kwenye mataa ya Koo? kwa nini washike mbele tu tena kwenye nanihii na isiwe mgongoni au kuyakumbatia kabisa mabega?

kwa nini wasanii hawa hupendelea kushika sehemu za siri na kuziminya kana kwamba zimewakosea kwa kiasi kikubwa na wanatoa adhabu?

ndivyo mziki wa kizazi kipya unavyokua kwa kufanya mambo ya ajabu ajabu tena kwa kuiga toka kwa akina P. Diddy na wenzie kina Snoop DogDog.

Ina maana akina P. Diddy wakila V-nye-C na wao watakula vya kwao? hayo si ndo mambo ya kuiga? si twaigan kila kitu toka magharibi? Wao washike nasi tushike ? wao wakisema Maza faka nasi twasema baza faka!

wakitembea mataa ya koo nje nasisi tutembee mataaa ya koo wazi eti tu kwa kuwa P. Diddy kaacha yake nje? utamaduni huu umeanza lini kwetu Tanzania?

Mjinga atakwambia huu ni ushamba, kwani mkiimba huku mnapeperusha mikono kama mnataka kupaa mbinguni bila kuipeleka kusini mziki hautachezeka?

Si mshike basi hiyo maiki kwa mikono mikono miliwi? mbona kuna staili nyingi tu za kucheza vizuri bila hata ya kumsumbua huyo jamaa?

kama mmeshindwa kubuni staili nyingine ni bora tu muwe wastaarabu kama mnacheza ngona ya Mganda maana hii ndiyo asili yetu watanzania.

huu ni ushauri wa bure kwenu nyie vijana wa vizazi vipya, kama hamtaki mtajiju, na kushikashika kwenu huko WALAH! mtajikuta siyo ridhiki!

Mnadhani huyo jamaa anapenda kuchezewa ovyo? Mazingira, tamaduni na makuzi yetuhayako hivyokizazi kinateketea kimaadili huku wanajua kuwa wanayoyafanya si mema machoni pa watu.

makabila mengine wanapoona mnashika hivyo kwao tafsiri yao ni matusi makubwa ya nguoni sasa mnafikiri watakuja hata kwenye hayo matamasha yenu watukanwe?

Badilikeni basi vijana wenzangu kwa kuwa huo mziki wenu hata mimi naupenda sana lakini naogopa kutukanwa pale mnaposhika chini, acheni kumfundisha Junior Tabia mbaya.

wasanii wa kizazi kipya na kile cha zamani bila kuwasahau wasomaji wote mnakaribishwa kutoa maoni yenu bila jazba wala upendeleo wa aina yeyote karibuni sana!

Wednesday, June 01, 2005

Kutoka Ugogoni

Hii ndio asili halisi ya Jina 'MATONYA'

AGWEE! MATONYA ta uze ahano luluhaba ukuchemwa siukusaka kuza, Sunheee!
WEE MAMVUA hebu njoo sasa hivi kwa nini unaitwa hutaki kuja? fanya haraka!

Jina la matonya ni maaruu sana hapa nchini watu wengi wakitajia matonga huwa wanahamisha mawazo yao na kufikiria mkoa wa Dodoma yaani naanisha UGOGONI!

Matonya ina maana kubwa sana na hasa wale wenyeji wa mkoa wa Dodoma wanalifahamu hili kwa sana! yaani wanajua kuwa kama hakuna matonya lazima mwaka huo kutakuwa na njaa.

Matonya ni mvua nyingi za masika mabzo zinanyesha kwa fujo katika kipindi cha msimu wa mvua husunani katika mikoa ya kanda ya kati.

Ni kipindi cha masika yaani mvua zilikuwa zinanyesha kama hazina akili nzuri vile.

Na mara nyingi watu wa majina haya huwa ni wanaume ambao ni akina matonya, lakini kwa upande wa wanawake waliozaliwa katika kipindi hiki huitwa 'Mamvula' yaani mamvua.

Agwe Leche Duh! wala sijakutukana naanisha wee acha tu! watu wenye asili ya majina haya hutokwa sana na jasho katika muda wote wa maisha yao.

Hutokwa na jasho katika wakati wa baridi na hata wakati wa joto wao hutokwa na jasho, awe mwembamba au mnene yeye anatoka jasho kwenda mbele yaani kwa ufupi hutaniwa kuwa wana afya sana.

Sasa nafikiri mpaka hapa kila mtu ameshaelewa nini maana halisi ya jina hili kwa kuwa kila jina lina maana yake watu wengi wamekuwa wakiyakataa majina yao ya asili na kusahau kuwa huo ni utukufu wa kimila.

Jivunie kabila lako kqwa kudumisha mila ili upate baraka na heri nyingi duniani!

Tuesday, May 31, 2005

JIFUNZE KUBLOG MTANDAONI

KWA YOTE HAYO BONYEZA hapa

Kusoma nje ya Nchi sio lazima usafiri nje ya nchi yako!

HAYA jamani kwa wale waliokariri kusoma nje ya nchi mpaka upande usafiri kwa kupanda ndege na kwenda marekani au Uingereza hapana.

Unasoma nje ya nchi wakati uko ndani ya nchi, na unapata Digree kwa muda wa miezi michache kama alivyonena kaka yangu hapa Bw. R.s Miruko.
kama unabisha bonyeza hapa.

Saturday, May 28, 2005

WANAWAKE BWANA...........! YAANI AKULETEA VIRUSI NA UNAVIPOKEA KWA MIKONO MIWILI

KAMA mkeo au mpenzi wako anatoka nje ya ndoa na unajua kabisa yaani una uhakika utafanya nini?

Jibu la swali hili kwa wanaume wengi litakuwa ni lenye kuashiria maumivu kwa upande wa pili.

kwa vipi sasa?

jibu linaweza kuwa nitamwacha hapahapo au nitamwua ama tutakufa wote mimi na yeye, hayo yanweza kuwa majibu toka kwa mwanaume ambaye amefahamu hilo.ni amjibu ambayo ni ya kishujaa eh!

iwapo mwanamke angeulizwa swali hili unadhani angelijibu vipi?

bila shaka angelijibuhivi; 'nitaondoka au nitamkomesha huyo hawara yake ama shauri yake mwenyewe mimi si nitaendelea na maisha yangu' haya ni majibu muafa ya kinyonge eh!

kwa kawaida wanaume hawako tayari kusamehe kosa la kutoka nje linapofanywa na wake au wapenzi wao, ni wachache sana wanaoweza kusamehe.

sisemi kwamba hakuna wanawake ambao nao huchukulia kutoka nje kwa waume zao kama jambo lisilo sameheka, kiwango cha wanawake hao ni kidogo sana ikilinganishwa na kile cha wanaume ambao hawako tayari kusamehe uzinzi wa wake zao ama wapenzi wao.

wanaume saba kati ya kila kumi hutoka nje, tafiti zinaonyesha kuwa wanawake karibu watano katika kila kumi wanajua kuwa wanaume wao htoka nje lakini huwa hawana la kufanya, wameamua basi!

alkini wanawake wanane katika kila kumi wanajua kwamba waume zao wanatoka nje na wanachukua hatua za kupambana na hali hiyo wakiwa ndani ya ndoa zao, wakati ni mwanamke mmoja katika kila wanawake kumi ndiye huondoka kwenye ndoa ya aina hiyo. hii siyo taarifa nzuri kwa akina mama.

KUKUBALI kuishi kwenye ndoa ambapo una uhakika kabisa kwamba mwenzako anakwenda nje kutafuta kifo huku akikufuja kwa njia moja ama nyingine ni kujishusha sana, kuna wale wanaosema shauri lake kwa sababu wameshakubali kwamba wao ni watumwa wa hao wanaume bila kufikiria.

hivyo wana haki ya kupangiwa nao hata siku ya kifo, hapa wanawake na wasichana ni lazima tuwe macho na tuamke sasa tukiendelea kuishi maisha ya namna hii matokeo yake tutakuwa tunasubiria kuletewa virusi vya UKIMWI na tunavipokea kwa mikono miwili na badae tunakufa kwa ugonjwa wa Ukimwi kwa madai kuwa Mungu katutenganisha.

Wednesday, May 25, 2005

Wachungaji hawa walichunga sana Kondoo wa Bwana.!

Eee baba Mungu wabariki hawa Nguchiro wafanikiwe kwenda kwenye adhabu yako ya milee wakiwa kama kuni katikakatika ya mafiga ili waungue vyema kutokana na kuudanganya uma kuwa wao ni wachungaji wa kondoo, AMEN.

Tuesday, May 24, 2005

TLP! Ni kaaazi kwelikweli.............!!!!!!!

HAKI ya Mungu yaani Chama cha Tanzania LabourTLP kina mbwembwe kweli kweli! Zile za CCM ni cha mtoto wanawake sasa sawa na wanaume yaani wee acha tu.

ni kwamba hivi karibuni chama hicho kimemsimamisha mgombea mwenza wa urais mwanamke ambaye atakuwa akigombea nafasi hiyo na Mwenyekiti wa chama hicho Bw. Augustino Lyatonga Mrema mwezi oktioba mwaka huu.

basi bwana wamemsimamisha mwanake awe mgombea mwenza wa nafasi hiyo kwa madai ya usawa unazingatiwa katika chama hicho ambacho hivi karibuni tuu kimepata ruzuku baada ya msajili wa vyama vya siasa nchini Bw. Tendwa kutangaza kuwa anakitambua chama hicho.

lakini sasa huyo mgombea mwenza anavigezo vya kuwania nafasi hiyo?

kwa kuzingatia yafuatayo wenyewe mtasema kama vigezo anavyo ama laa!

* Je Ikulu ni Maabara ya kufanyia majaribio ya uongozi?
* Ikulu ni mahali patakatifu amejitakasa?
*kazi ya urais si ya kubeba zege Bongo yake inachemka?
*utamu wa komamamnga ni komamamnga lililokomaa, amekomaa?

Angalizo: USHUZI HAUZIMI MOTO! Mnakaribishwa kuchangia maoni yenu bila woga wala Jabza na kutopendelea kwa aina yoyote, karibuni sana.

Friday, May 20, 2005

Takrima ni tatizo la Kimaumbile

Najua kila mtu ana hamu ya kulifahamu hili kwa undani kwa nini takrima iwe tatizo la kimaumbile ni maelezo machache tu hapa mda mchahe utakuwa umeelewa.

ni hivi ; kwa mujibu wa mila na desturi za kitanzania ni kwamba mtu anajikuta mwili unamuwasha kila anapokuwa anasalimiana na wenzake hapa naamanisha viongozi mbalimbali hapa kwetu tanzania.

hii inawatokea mara nyingi katika nyakati mbalimbali na hasa katika nyakati hizi ngumu za uchaguzi pale wanapojiandaa kutafuta kura katika kampeni zao.

anajikuta mwioli unamuwasha, anajikuna kwa staili ya kuingiza mkono mfukoni akitoa anatoa burungutu la pesa, anawagawiwia wapambe na wapiga kura akiwa hajitambui kabisa kuwa anawashwa anajikuna kwa staili ya aina gani.

akimaliza kujikuna anarudiwa na fahamu na kukumbuka kuwa alitoa burungutu la pesa na kuwagawia watu mbalimbali na kugunduia kuwa ametoa takrima, basi tena ndo matatizo ya kimaumbile na staili za kujikuna pale unapojisikia uanawashwa.

TAKRIMA NI TATIZO KUBWA SANA LA KIMAUMBILE SASA ANATAFUTWA DAKTARI BINGWA WA MAGONJWA YA NGOZI ASAIDIE KUTATUA TATIZO HILI KWA WATANZANIA KWA KUSHIRIKIANA NA TAKURU.