Monday, May 16, 2005

He! Kumbe kuna watu wanakunywa pombe kila siku lakini hawafahamu bei yake........

Ni ngumu kuaminishwa lakini utakaposhuhudia ni lazima ukubali kuwa ni kweli yanatokea.

hii kwa wale wahudumu wa sehemu zinazouzwa Pombe yaani 'Bar wanalitambua sana hili na wala sio geni kwao kutokana na uzoefu wa kazi yao ya kuuza bia kwa watu mbalimbali.

wahudumu wao ambacho hujali ni kulipwa pesa zao haijalishi pesa hiyo ni ya wizi au ya kuhongwa kitu ambacho kimekuwa kikiwagharimu wanunuaji au walipaji wa vunywaji husika.

hapa kubwa ninalolizungumzia ni kuhusiana na tabia ya baadhi ya watua mabo kila mda ukikutana naye kila muda yeye amelewa tu halafu kabla ujamuuliza utasikia anakwambia niko pombe anadhani ni sifa kubwa mbele ya watu anaowambia.

lakini cha kushangaza ni kwamba mtu huyohuyo ukimuuliza umekunywa ngapi kwa sauti kubwa atakujibu harakaharaka nimekunywa kumi, na ukimuuliza ni sawa na kiasi gani cha pesa alichotumia utamuona anainama chini kana kwamba anafikiria kitu cha maana badala yake anakujibu SIJUI.

NI hatari sana kwa wale wenye tabia hii hususani ni akinaada ambao kutwa yuko pombe ukimuuliza bei ya bia moja hajui ni kiasi gani akian kaka nao tabia hii ni hatari sana zaidi kuliko kwa akina dada, lakini haya si mawazo yango hata R.S analitambua hilo.

Hebu tuweni na ustaarabu jamani hata kama unapewa ofa kila siku basi siku moja pita mwenyewe bar ujaribu kuulizia bei tu ya bia kama unavyofanya kwenda dukani kuulizia bei ya kiatu au nguo ili uwe na uhakika wa ofa unazopewa mtaani.

No comments: