Monday, May 02, 2005

TOP 5 wa sensitine ndogo ya Nec hawa hapa!

Haki ya Mungu yaani huwezi kuamini mambo CCM yaani chama cha mapinduzi, watu wote sasa masikio yao na akili zao zote zimeelekezwa mjini Dodoma kwa ajili ya kujua ni nani atakayepigana kiume kufa na kupona kwa ajili ya kumrithi Mkapa.

Kubwa ambalo hata wenyeji wa mkoa wa Dodoma ambao pia nao ndi wanaishi hapa mbado wana hamu ya kuwafahamu hao waliofanikiwa angalau kuonja kidogo hayo ambayo kwa pia wanahisi ni mafanikio ya kuanza safari ya kwenda Sensitine Kubwa ya Chimwaga.

akina mama nao hawako nyuma, wako msatari wa mbele kwa ajili ya kufanikisha akina baba ambao walijitokeza katika kuonja majaraibio ya kinyan'ganyiro hicho wanafanikiwa na wao kuitwa 'FIRST LADY' licha ya kuwa wao waliogopa kluchukua fomu na kuongozana na waume zao ambao hapo baada nafikiri wangeitwa 'FIRST GENTLEMAN'

mpaka sasa wachezaji 11 wako uwanjani wakiongozwa na golikipa Babu Ushindi ambaye kwa mujibu wa wataalam wa mambo ya siasa anatisha kimsingi.any way kesho utawafahamu hao TOP 5! USIKOSE!

1 comment:

Rama Msangi said...

Acha kutuyeyusha wewe, blogi sio magazeti ya Bongo ya Udaku