Thursday, May 05, 2005

MAPAPARAZI wapewa vitambulisho vya Wahudumu!

Waandishi wa habari ni watu muhimu sana hapa nchini na duniani kote kwa ujumla na wengi wamekuwa wakiita fani ya uandishi wa habari kuwa mhimili wa nne!

lakini watu hawa wamekuwa wakionekana kuwa hawana maana sana na hasa pale wanapoalikwa katika shughuli mbalimbali za kitaifa.

Ni hivi karibuni mjini Dodoma kulimalizika tukio kubwa ambalo lilikuwa linakamilisha neno kutimia ambapo wana CCM walikuwa wakiteua mgombea urais ambaye wengi wanaamini huyo ndiye rais wa awamu ya nne.

katika mkutano mkuu huo maalum wa CCM wageni wengi toka ndani na nje ya nchi walialikwa kwa ajili ya kuhudhuria mkutano huo wakiwemo waandishi wa habari toka vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini.

licha ya kualikwa kwa wageni wengi na waandishi pia, wageni hao walitafutiwa mahali pazuri pa kulala na kupewa kadi maalum za kuingilia katika ukumbi wa mikutano wa CHIMWAGA.

kinyume na wageni wengine waandishi wa habari hawakupewa uzito kama ilivyokuwa kwa wageni wengine ambao walialikwa kuhudhuria Mkutano huo na badala yake walionekana kama wafanyabiashara wa nguo toka mikoani.

siku ya mkutano baadhi ya waandishi wa habari walionekana kukosa kabisa kadi hizo maalum ambazo walitakiwa kuwa nazo na kuwaruhusu kuingia katika mkutano huo maaluma ambao ulikuwa na ulinzi kupita kiasi.

baadhi ya waandishi wa habari na wapiga picha ambao walibahatika kunusa milango ya ukumbi huo walipata kadi za uhudumu wa Vinywaji na vyakula ambazo zilkuwa zinatumiwa na wauzaji wa vyakula na vinywaji nje ya ukumbi huo.

hii iliniuma sana, mbaya zaidi ni pale matukio muhimu yaliyokuwa yakitokea ndani ya ukumbi huo yalikopokuwa yanafanyika wapiga picha na waandishi wa habari walitakiwa kushuhudia ili kuwapa taarifa wananchi ambo wako tandahimba.

ilikuwa ngumu kwao kuingia kutokana na vitambulisho vyao kuwaruhusu waandishi na wapiga picha kuishia nje ya milango ya ukumbi huo.

kilichokuwa kinagomba hapa ni kwamba baadhi ya maafisa wa usalama walikuwa wakiwaambia waandishi hawa kuwa "nendeni mkawahudumie huko nje huku ndani tuko kamili"

licha ya kunyimwa vitambulisho pia walifukuzwa katika nyumba za kulala wageni amabzo walikuwa wamefikia kwa madai kuwa CCM ilikuwa imezikodi nyumba zote kwa ajili ya kufikia wajumbe wa Cma hicho.

hii inaonyesha ni jinsi gani waandishi wa habari wasivyothaminiwa katika jamii hususan na baadhi ya viongozi wa Chama cha mapinduzi katika idara ya habari.

CCM kama hamuyawezi waachieni Idara ya habari maelezo watayamaliza wao bila kufanya hiyana kama mliyofanya katika mkutano wenu mlitukwaza sana.

Tumewasamehe na tumemkemea Pepo mchafu aliyemo nsdani ya chama chenu katika jina la Yesu ashindwe na asiendelee kuwepo! AMINA.

No comments: