Saturday, April 30, 2005

Kutoka Ugogoni

Namaanisha kutoka kati kati ya Tanzania, katika mkoa unaokwenda kwa jina la Dodoma (zamani Idodomya), mkoa ambao toka miaka ya kupata uhuru wa Tanganyika (sasa Tanzania), viongozi wetu wamekuwa wakiota kuufanya makao makuu ya nchi hii, ingawa ndoto hii ya viongozi wetu wakuu, imeendelea kuwa kuukuu kwa zaidi ya miaka 40 sasa.

Naam, huko ndiko anakoibukia binti huyu wa Kitanzania, ambaye kwa jitihada nyingi za binafsi na za washauri mbalimbali, ameamua kuvamia ulimwengu wa Blogi. Ujumbe wake kwako ni kuwa, anajua kwamba itamchukua muda sana kuweza kufikia hatua za juu sana katika teknolojia hii, lakini haidhuru anaamini ipo siku atafika kwa msaada wako na wa wengine pia.

Hii ni nuru kutoka kwa Wagogo, kabila kuu katika ukanda anakotoka mwanablogi huyu, japo nalo pamoja na kuwa kabila kuu, bado hali yao imeendelea kuwa kuu kuu kwa miaka nenda rudi. nani ajuaye, huenda siku zao za ukombozi ndio zimeanza leo hii, tusubiri tuone.

Shukrani kwa wote mliokuwa na hamu ya kuona mtu kama mimi naibuka kwa ajili ya ninyi kuniunga mkono.