Wednesday, June 01, 2005

Hii ndio asili halisi ya Jina 'MATONYA'

AGWEE! MATONYA ta uze ahano luluhaba ukuchemwa siukusaka kuza, Sunheee!
WEE MAMVUA hebu njoo sasa hivi kwa nini unaitwa hutaki kuja? fanya haraka!

Jina la matonya ni maaruu sana hapa nchini watu wengi wakitajia matonga huwa wanahamisha mawazo yao na kufikiria mkoa wa Dodoma yaani naanisha UGOGONI!

Matonya ina maana kubwa sana na hasa wale wenyeji wa mkoa wa Dodoma wanalifahamu hili kwa sana! yaani wanajua kuwa kama hakuna matonya lazima mwaka huo kutakuwa na njaa.

Matonya ni mvua nyingi za masika mabzo zinanyesha kwa fujo katika kipindi cha msimu wa mvua husunani katika mikoa ya kanda ya kati.

Ni kipindi cha masika yaani mvua zilikuwa zinanyesha kama hazina akili nzuri vile.

Na mara nyingi watu wa majina haya huwa ni wanaume ambao ni akina matonya, lakini kwa upande wa wanawake waliozaliwa katika kipindi hiki huitwa 'Mamvula' yaani mamvua.

Agwe Leche Duh! wala sijakutukana naanisha wee acha tu! watu wenye asili ya majina haya hutokwa sana na jasho katika muda wote wa maisha yao.

Hutokwa na jasho katika wakati wa baridi na hata wakati wa joto wao hutokwa na jasho, awe mwembamba au mnene yeye anatoka jasho kwenda mbele yaani kwa ufupi hutaniwa kuwa wana afya sana.

Sasa nafikiri mpaka hapa kila mtu ameshaelewa nini maana halisi ya jina hili kwa kuwa kila jina lina maana yake watu wengi wamekuwa wakiyakataa majina yao ya asili na kusahau kuwa huo ni utukufu wa kimila.

Jivunie kabila lako kqwa kudumisha mila ili upate baraka na heri nyingi duniani!

No comments: