Friday, March 05, 2010

HIZI NI SALAMAU ZA WAGOGO KUTOKA KWA KAKA FREDIRICK MUMBULI!

Da Martha,

Nimefurahi kuona kazi nzuri unayoifanaya, ni Tuvuti nzuri ikieendelezwa na ikapata habari nyingi moto moto.

Kumekuwa na jitihada nyingi kukujaribu kuwakumbusha na kuwahamasisha Wagogo kuungana na kufanya kazi za maendeleo na hususani za kiuchumi (Ujasiriamali) lakini nyingi ziko kwa mwendo wa kinyonga, Wanyausi wamebaki na kilio cha Ukame (Chibahu) na umasikini!

Leo hii ukijitambulkisha mgogo haraka kwenye mawazo ya “wanyamunthu” kunakuja wazo la omba omba/masikini, siku hizi tumewafunika hata watani zetu, maana sisi tuna hata mbwembwe za aina aina za kuomba! Lakini kwa nini, au kuna nini vichwani mwa wanyausu?

Kwa nini tusizinduke sasa, mbona wakati tulalamika ukame na umasiki uliokithiri, shemeji zetu Wachaga wanaporomosha majumba ya magari ya kifahari, kwani hivi wanavuchumia wapi! Mbona waheshimiwa kutoka kondoa wanachangamikia tenda, sisi tumebaki “usiku wo monga!”. Haya sasa Vyuo hivyo, wanakuja watoto wa wenzetu wanapata elimu wanarudi kutumikia makwao, hata kama kuna wazalendo wanachuma wanaenda kujenga kwao na baadhi wanawekeza Dodoma.

Wanyausi wana nini, mbona wapo kama wameridhika tu na maisha duni! Tumesikia madinai yalipatikana maeneo Fulani huko Mpwawa wamekuja wenzetu wajanja wakachota, hata huko Wilaya mpya kunatetesi chini kuna mali, badala ya kushiriki midahalo na mijadala mbalimbali nasikiwa wanyausi wameshafyata mkia wao wanafikilia Matembe yao wataenda kuyaotesha wapi!

Wanyausi, Zabibu! Wataliano huko Homboro wanabweda tu, hebu jaribu kuulizia Mvinyo wa Homboro kama utaupata kwa urahisi hapa nchini labla uende majuu Hongera Wanyausi wa Chinangali kuanzisha tena zao la zabibu, lakini angalieni isiewe nguvu ya soda! Kwani hamkumbuki enze za zabibu Mlowa bwani, Kigwe na kungineko vijiji vilinunua mpaka Malori, magari na mashamba hayo vikowapi.

Hongera ndugu zangu wa Mbabala! Kumbe tukiwezeshwa tunaweza, sasa hebu CRDB iingalie na Miradi mingine, kama Ubuyu, unashanga! Hebu tukikusanya maauzo yote ya ubuyu Dalisama tu, mboana watu wanalipa kodi na ada za shule” nkani ya mapela” Mazao kama Alizeti, ufuta na karanga yakiwezeshwa, mashudu tutalisha ng’ombe, na mbuzi wataongezeka mnadani.

Wanyausi, sasa tena hata Nindo, Msunyunto, Muheme, Chipande, Masembegu Chiganda, taja…… hatuvisamini tena, si hata tungetengeneza Single na sisi tukatoka Maanderground! Mbona inawezekana, mbona Dada yetu kavaa koti ya Chimuli akatoka naye alitoka Tanga.

Kaka zangu Mavunde na Yobwa, papa Mchoya yuko wapi? Najua kazi nzuri za huko St. James Arusha, UVUKE-DodoMA, taja.............. Mvua hainyeshi, mbona kumeanzishwa kiwanda cha maji, Sante! Kwani maji ya mzakwe yameisha, mto Bubu vipi sikuizi unaongea, hayo maji tuyafate huko huko chini, Hiviiiiiiii mbona Waarabu hawahami jangwani, sisi kila siku mabasi kwa basi DALISALAMA, tunawaachia wenzetu nyumba, mnategemea nini!

Si ajabu waheshimiwa hawataki kuhamia Dodoma maana wanashanga nyie mnawambia wahamie Dodoma, lakini mnapishana nao Dumila, mkienda Dalisalama, nyinyi mnakimbia nini, halafu mnawazimisha wahamie Dodoma, hiviiiiiii mmesahau usemi wa Wanyausi “Mnyanyumba sangalale……..” Y ako mengi yakusema, lakini iko haja ya wanyausi kufikiria tena, Dodoma tunamwachia nani, Mzee mkubwa, Baba, Koko wewe tu umebaki kati ya Wazee wetu, hivi mkikaa na Mzee mwenzio hamweza kutuamusha, mwene chibede cha chichi! So chi wayangu! Sema neno moja tu mbona tunakuaminia.

Sasa hebu angalia wageni wanakuja sisi tunatoka kwenye vibarua Dalisalama, hata kweli ni adamu ya “KWI KUMBU” tuliojifunzo, ng’o yai! George Kusila alinza kitu cha Wanyausi kuwakumbusha walikotoka, basi hata wakishindwa mengine, miili tu irudishwe ikazikwe kijijini, hata hilo nalo limekuwa gumu, hiviiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii! Kalumbu asante sana, kwa wasaa huu naomba nikukaribishe kikao cha wanyausi 14/02/2010 Dalisalama , tunapanga sehemu ya kukutana ukinipigia baada ya kesho nitakuwa na jibu.

Wakutya Wagogo chili Chibede, chili machela vitatufikisha wapi ndugu zanguni! Salaam.

from Freddy Kapande (Kigwe) mumbuli@yahoo.com 0715327683

3 comments:

Martha Mtangoo said...

KWA kweli kaka Mumbuli uko juu haya yote uliyoyaongea hapa ni kweli kabisa, kwa sababu mi naongea hapa kama mgogo kweli wagogo cili chibede muno muno!tukipunguza Chibede angalau mambo yanweza kuwa shwari, asante kaka mumbuli kwa mawazo mazuri karibu tena.

Anonymous said...

Decide to be a good person who will not be evil.
Inherent in the offer of clone hosting is a clue:::"Earn" by hurting others. This violates this vow, causing people to incurr evil, and the clue you need to avoid it. Sadly, as young people too many are still corrupted, still unenlightened and make the mistake when offered.
Only innocent pure children ascend into heaven, while evil is relegated to entering clone hosting, where they are reincarnated as lesser life forms. One day the Christian Rapture will be used as a "consolation prize", and usher in the era of compensation according to the Bible:::1000 years with Jesus on Earth.
Everlasting life with Jesus, but only for true believers:::Placement to suffer on the next Planet Earth punishment for worshipping a false god.

"Some people are evil." This is the gods fulfilling people's history by pushing them into that legacy. This is the gods accepting culpability and blame with their participation.
As we devolve and approach The End the gods transition to temptation, deceiving them into thinking they are "earning", allowing them to wash their hands of culpability. As this occurrs for more of us in society the gods are preparing for the Apocalypse, for when The End comes the gods will not be to blame for the result.
The disfavored think the opposite, that now that they are participating they have favor, and they will live forever because of it.

1.14
9:20a
Talk of Republicans unwillingness to raise the debt ceiling. They insist on spending cuts.
As inefficent as government has been allowed to become perhaps we should begin with the size of government and look to their own support staff. Sacrifice needs to be made by all. I am concerned there is nepotism and favoritism occurring in these support jobs, and the size gets out of hand because of it. I would expect these Republicans would not be willing to look within their own offices.
Federal and state governments is very much like the farmer and his water allocation:::To continue to achieve increasing allocations they would rather discharge the water rather than report underuse.
Perhaps if I worked at the Department of Education in Pleasant Hill some progress could have been made, a framework allowed by this preditory DM. But watching them instruct the clone host fakes in the Federal government to hold out and force the consservative Democrat Obama to look bad illustrates teh Antients have made up their minds and intend to force it.

The gods may share some values of the conservatives (mostly good, a little evil), with the exception of capitalism, warmongering and environmental degredation, but they also share in the economic degredation of the conservatives which will bring the United States to bankrupcy and anarchy. It initiated with Ronald Reagan taking the National Debt from $1T to $6T.
And me, the hundred billion dollar man, will have to meekly ask for a nice apartment (conservative timeshare dream).
As long as the gods have this vested interest of the Situation they are calling the shots. They order all proceedings to ensure they get what they want. This is not to say they will transistion when it is over, but I suspect this final absolution of culpability is necessary for them to completely wash their hands of Earth in preparation for the Apocalypse.

The gods gave you AIDS in Africa to correct your promiscuous sexual behavior, just as they did with the homosexuals in the United States in the 1980s. They used those who destroyed life on Planet Earth to do their legwork, as they did with most other important elements. This way they managed their culpbaility, are not to blame and can walk away cleanly.

Paul charles said...

Mimi ni mgogo nimezaliwa mkoa wa kilimanjaro baba yangu (CHARLES SULUT SAMVUGA)alitoka dodoma miaka ya 1980s ndipo alipokutana na mama yangu nikazaliwa 1997 akafuata mdogo wangu,baba alifanya kazi ya ulinzi katika kituo kimoja cha mafuta kuanzia miaka hyo hakuwai kurud dodoma kwa miaka yote mpaka mwajiri wake aliyemleta akafariki aliendelea kukaa pale takriban miaka mitatu ndipo mungu akamchukua 29 march 2019 nimebaki njia panda maana sijui naanzia wapi sikuwahi kuwajua ndugu zangu kwa maelezo yake alizaliwa maili moja na hata mila za wagogo sizifahamu naomba ushauri dada yangu.