Tuesday, July 05, 2005

Kwa Nini Sisi Tuweze tuna Nini na Nyie mshindwe mna nini? Mnannisikitisha sana, nyingine mpya hii hapa!!!!!!


NASIKITIKA sana kuona eti asilimia 95 ya Mablogist wa Kiswahili ni Waandishi wa Habari kwa nini lakini?

Mbona mnaifanya mioyo yenu kuwa migumu jamani, Kublog kiwahili sio dhambi, na kama siyo dhami haiwezi kuleta mauti zaidi ya kukupatia faida jamani kwa nini?

kama mnadhani mimi muonugo Fungua Blog nyingine hii hapa www.ngurumo.blogspot.com uone nini kunaendelea.

huyu anaitwa Ansbert Ngurumo ni Mwandishi wa habari Mwandamizi na Nzuri zaidi ni Mhariri wa Gazeti la Tanzania Daima Jumapili, kwa nini basi Madaktari, Maprofesa au hata Wakulima ambao vijiji vyenu vinaendelea mshindwe kuanzisha Blog zenu jama?

wala haihitaji fedha kwa ajili kuanzisha na kumiliki Blog, nawaombeni jamani Bogo si kwa ajili ya Waandishi wa habari ni kwa yeyote Mwenye nia ya kumiliki. msiogope jamani tafadhali msiogope.

1 comment:

Indya Nkya said...

Tatizo ni kwamba watanzania tunadhani kazi ya kuhabarisha umma ni ya waandishi wa habari tuu.