Wednesday, July 27, 2005

KHA! Akina dada Tumelaaniwa au?


NAJUA, kuwa kila mtu anayetyembelea Web Page yangu anafahamu kuwa ni nini naongelea zaidi katika kila kurasa.

Sasa hili nililokutana nalo linaniytia uchungu sana, inaniuma sana ninapoona akina dada wenzangu wanafanya mambo ya ajabu wakati wamejaaliwa kila kitu yaani wamekamilika kila Idara.

Hebu angali sasa ni nini hiki? inaiuma sana kuona akina dada hatujithamini kabisa miili yetu, eti siku wanasema wapewa bure na lazima wapewe bure wewe usijidanganye kwa hilo na ulaaniwe.

Huyu ukimuuliza ni nini anafanya hapo atakwambia yuko kazini lakini hiyo kazi yako ya kucheza shoo ukivaa vizuri mbona itanoga tuuu? kilichomsibu sasa Soma hapa chini.


Mr Nice nusura amtwange mnenguaji wake!

MWANAMUZIKI mahiri katika miongoko ya Takeu ya kizazi kipya Lukas Mpenda almaarufu Mr Nice Ijumaa iliopita alimkwida mnengaji wake aliyetambulika kwa jina la Mpasi Mussa nma almanusura angemtwanga makonde.

Tukio hilo lilitokea kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa bendi ya Msondo Ngoma Music ambayo zamani ilikuwa ikiitwa OTTU Jazz. Mr Nice alimkunja mnenguaji wake akionekana kapndwa na hasira kitendo kilichofanyika nyuma ya jukwaa la ukumbi huo uliokuwa umehudhuria na mashabiki wengi.

Mr Nice alizua tafrani hiyo kwa madai kwamba mnenguaji wake huyo alikosa nidhamu kwa kudai pesa yake kwa utaratibu aliodai haukuwa wa heshima. "Inabidi nikuonye kutokana na utovu wa nidhamu ulioufanya, nakuonya kama mdogo wangu," alisikika akifoka Mr Nice.

Hata hivyo menguaji huyo aliomba msamaha na ndipo Mr Nice alipomwachia huku akisikika akimwambia: " Mimi sipendi kufanya kazi na watu kama nyinyi, sitaki kuwa pamoja na wewe kwa sababu umenidhalilisha."

Acha kazi kwani lazima ucheze Shoo? anza hata kuuza Vitumbua au Maandazi ukiwa na Msimamo maisha yatakunyookea mwenyewe utashangaa huwezi kuamni.

Haya kila la Kheri

1 comment:

Anonymous said...

Ni bora watafute chumba wamalize kazi yao! Eti ndo shoo hii! Aibu kweli kweli!