Monday, May 09, 2005

'FIRST LADY' Huyu hakupata kitchen Party kabla ya Kuingia Ikulu?



KILA mtu anaamini kuwa Ikulu ni mahali patakatifu na kila anayeingia Mahali hapo alzima awe ametakaswa kabla hajaingia, licha ya kuwa ni ngumu mtu kutakaswa kabla hajafa.

suala la kujitakasa pia ni zuri na hasa kwa akina mama ambao wana madaraka makubwa ya kuwaongoza wenzao au akina mama ambao waume zao wana madaraka makubwa hii ikiwa ni pamoja na kuwa mke wa rais.

nawapa pole sana wenzangu wakenya, hapa naamanisha watu wote wanaoishi kenya Afrika mashariki hii ambayo tunategemea kuwa na Jumuiya ya afrika mashariki kwa kuchangia kila kitu hususan katika masuala ya biashara.

pole hii hasa ni kwa akina mama wa kikenya, nawapa pole sana hawa kwa kuwa mke wa rais waoamekuwa akifanya mambo ya ajabu ikiwa ni pamoja na kushinikiza mumewe kufanya mambo ya ajabu ajabu kutokana na mumewe kuwa na cheo cha juu cha utumishi kuliko vyeo vingine hapa afrika.

mama huyu licha ya kufanya mambo ya ajabu hivi akribuni alitoa kali baada ya kuvamia chumba cha habari cha gazeti moja la nchini kenya akitaka kuombwa radhi kutokana na gazeti hilo kumuandika.

licha ya kuvamia chumba hicho cha habari pia mama huyo alimpiga vibao mpiaga picha wa gazeti hilo kwa madai kuwa alimpiga picha!

sasa mablogist wanawake wenzangu kwewli hii ni haki? mwanamke mzima mwenye akili timamu na mumeo ni mtu mwenye madaraka ya juu unafanya mambo kama mtoto mdogo anayesoma vidudu?

poleni sana akina mama wa kenya huyu mwanamama amewadhalilisha sana akinamama wa kenya kwa tabia yake hiyo ya ajabu kwa kufanya hivyo watu wa mataifa mbalimbali wamefikiria kuwa wanawake wa kabila lake wote wako kama mama huyo alivyo. pole sana First Lady! milango iko wazi kwa ajili ya kuchangia maoni yenu kuhusiana na tabia ya mama huyu wa ajabu karibuni wanablog.

No comments: