Thursday, May 05, 2005

Ni moshi wa kijani lakini sio wa Mjomba.............!

HAYAWIHAYAWI sasa yamekuwa, jana mosho wa kijani ulifoka katika ukumbi wa Chimwaga na kuwamwaga wale 2 ambao walitakiwa kumwagwa haraka sana kabla Jogoo halijawika.

hatimaye jana neno likatimia! shangwe na vilelegele vifijo na Nderemo nguo za kijani, moshi wa kijani hii ilikuwa ikimaanisha sasa Imekwisha.

kilichonitia wasiwasi ni pale Moshi ule wa kinai uliotoka na kuonnyesha aliyekuwa amechaguliwa ni mwingine siyo mjomba wangu! hapa ilikuwa ni ngumu kuamini lakini baadaye fahamu ziliponirudia nikaamini kuwa ni kweli hakuwa Mjomba.

lakini kwani huyo na mjomba wana togfauti gani hapa nilijiuliza na kukosa jibu kabisa lakini nilipomuuliza Binamu akaniambia kuwa eti mjomba alikuwa Mzee sana kuliko huyo mteule.

nikamuuliza Binamu kwani Ikulu kuna kazi za kubeba Zege? akanijibu kuwa hata kama kazi si za kubeba zege lakini huu ni muda wa vijana kuonyesha ujana wao katikia wakati wao wa ujana hususan ni kipindi hiki.

sikuishia hapo nikamuuliza tena; kwani ukienda katika kijiji ambacho umgeni sana utatafuta kijana maarufu au Mrembo maarufu na kuuliza shida yako?

akajibu hapa, nikamuuliza tena utumtafuta nani na kumuuliza? akijibu; nitamtafuta Mzee maarufu na kumuuliza.

hapo nikaridhika kumoyo! nataka kukwambia Binamu kuwa sasa kwa taarifa yako Mjomba amekata rufaa! na Ikulu hakuna kazi ya kubeba Zege na utamu wa embe ni lile ambalo limeivia juu ya mti siyo la kuvundika.

No comments: