Friday, May 20, 2005

Takrima ni tatizo la Kimaumbile

Najua kila mtu ana hamu ya kulifahamu hili kwa undani kwa nini takrima iwe tatizo la kimaumbile ni maelezo machache tu hapa mda mchahe utakuwa umeelewa.

ni hivi ; kwa mujibu wa mila na desturi za kitanzania ni kwamba mtu anajikuta mwili unamuwasha kila anapokuwa anasalimiana na wenzake hapa naamanisha viongozi mbalimbali hapa kwetu tanzania.

hii inawatokea mara nyingi katika nyakati mbalimbali na hasa katika nyakati hizi ngumu za uchaguzi pale wanapojiandaa kutafuta kura katika kampeni zao.

anajikuta mwioli unamuwasha, anajikuna kwa staili ya kuingiza mkono mfukoni akitoa anatoa burungutu la pesa, anawagawiwia wapambe na wapiga kura akiwa hajitambui kabisa kuwa anawashwa anajikuna kwa staili ya aina gani.

akimaliza kujikuna anarudiwa na fahamu na kukumbuka kuwa alitoa burungutu la pesa na kuwagawia watu mbalimbali na kugunduia kuwa ametoa takrima, basi tena ndo matatizo ya kimaumbile na staili za kujikuna pale unapojisikia uanawashwa.

TAKRIMA NI TATIZO KUBWA SANA LA KIMAUMBILE SASA ANATAFUTWA DAKTARI BINGWA WA MAGONJWA YA NGOZI ASAIDIE KUTATUA TATIZO HILI KWA WATANZANIA KWA KUSHIRIKIANA NA TAKURU.

1 comment:

Indya Nkya said...

Mambo mazito hayo!! huyo Daktari lazima atoke Mars hapa duniani hawajagundua tiba hiyo.