Thursday, May 05, 2005

"Hata nisipochaguliwa nitarudi kuwashukuru"

Hapa namnukuu aliyekuwa mmoja kati ya wale wanaiomba CCM kumteua kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho alipokuwa akirudisha fomu ya kuomba baraka hizo

Mgombea huyu alisema kuwa iwapo hatobahatika kupata nafasi hiyo ya kuteuliwa na kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho basi angerudi katika mikoa yote 26 aliyozunguka wakati akiomba wasdhamini kwa ajikli ya kumdhamini katika suala zima la kupata baraka za kuteuliwa kuwa mgombea urais.

alisema kuwa angerudi na kuwashukuru wale wote waliomdhamini na kuwataarifu matokeo juu ya kile kilichotokea katika uteuzi huo.

swali? je ni kweli atafanya hivyo!

nafikiri itakuwa ngumu sana kwanza bado anazo nguvu za kwenda huko kuzunguka na kuwatafuta tena wadhamni wake na kuwakatia takrima kama alivyofanya hapoa awali alikwenda kuwabembeleza kwa ajili ya udhamini?

nasubiri sana huu wimbo urudiwe kuimbwa na mwasiasa huyu ambaye alipokuwa akiyasema haya alionyesha ujasiri wa hali ya juu kana kwamba alikuwa an uhakika wa kuwa mteule katika nafasi ya kuwa rais mgombea.

haya tunakusubiri kwa hamu sana baba! wadhamini pia wana hamu ya kujua yaliyokusibu mpaka ukachinjwa na kutupiliwa mbali.

WELCOME BACK utupe FEEDBACK!

1 comment:

Indya Nkya said...

Kama hajapitwa na wakati anaweza akarudi ili mwaka 2015 akichukua fomu asipate shida ya wadhamini