Sunday, May 01, 2005

Wanawake wasubiri 'moshi wa kijani' Chimwaga

Licha ya ukweli kuwa hakuna hata mmoja aliyejitokeza kwa ajili ya kuwania kuteuliwa kuwa mgombea wa kiti cha urais kwa tiketi ya CCM, bado wanawake nchini Tanzania, kama walivyo Watanzania wengine watakuwa wakisubiri kwa hamu kujua kuwa baraza la mapapa wa CCM litafukiza moshi wa aina gani baada ya vikao vyao vitakavyofanyika katika siku tatu zijazo mjini hapa.

Kwamba kutatoka moshi wa aina gani, hilo sio swali ambalo mtu anaweza kulijibu kwa haraka sana hasa kwa kuzingatia kuwa karibu wagombea wote wana nafasi sawa ya kuweza kushinda licha ya tambo, mbwembwe na madoido ya hapa na pale yaliyoshuhudiwa toka kwao toka walipochukua hadi kurudisha fomu.

Je ni moshi wa kijani, wa njano, kijani na njano, moshi mwekundu kama alivyosema kakayangu Kulangwa au ni cheche kama alivyosema kaka yangu Rama? Swali hili litajibika hivi karibuni baada ya baraza la mapapa wa CCM kukutana pale 'Sestine' yao (Chimwaga). Tuombe kheri na Mungu atuongoze.

1 comment:

Ndesanjo Macha said...

Karibu sana dadetu Martha. Uwanja ni wako, wakimeza wakitema shauri yao. We chanja mbuga!